2017-02-09 17:00:00

Tulinde hazina ya maisha ya mtu kwa kupinga aina zote za vurugu


Ninawakaribisha na kuwashuruni kwa maneno yenu mliyotoa.Ni maneo ya Baba Mtakatifu Fancisko wakati wa kutoa hotuba yake kwa wawakilishi wa Kamati ya kupinga kashfa, akisema , watangulizi wake wa kwanza Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili na Benedikto wa kumi na sita walikuwa wamekwisha kutana na wawakilishi wa kikundi chenu, ambao kuna uhusiano  wa muda mrefu wa  Vatican tangu kipindi cha Mtaguso wa Pili wa Vatican .
Ninatambua na kufurahi ya kwamba mahusiano hayo yameendelea kwa kina ,na kwamba kama mlivyoeleza  juu ya mkutano wenu, ni ushuhuda muhimu na zaidi ya hayo ni majukumu , kwa nguvu ushirikiano unaleta uponyaji na kueneza mahusiano,kwa namna hiyo ninawashukuru na pia Mungu naye anafurahi kuona urafiki wa kweli wa kindugu kati ya wayahudi na wakristo. Ni kama isemavyo zaburi ya 113,1.3 ni jinsi gani ndugu wawili kuishi pamoja kwa manai  maana pale Mungu anatoa baraka na maisha daima.


Kama utamaduni wa makutano na maridhiano huzaa maisha, na kuleta matumaini, kinyume na kuwa na utamaduni wa chuki upanda kifo na mavuno yake ni kukata tamaa. Baba Mtakatifu anatoa mfano  kwamba mwaka jana amekwenda katika makambi ya mateso na ukatili huko Uholanzi (Birkenau). Hakuna maneno na mawazo ya kutosha kueleza tukio la namna hii ya ukatili dhidi ya wayahudi , bali ni sala kwa Mungu aweze kutoa huruma kwaajili ya majanga ya namna hiyo na yasirudiwe mara nyingine tena.Kwa njia hiyo tutaendelea kusaidiana moja baada ya mwingine , kama wito wa Mtakatifu Yohane Paulo wa pili  alivyosema naye kwamba, "katika kufanya kumbukumbu ya utekelezaji wa majukumu, ni muhimu katika machakato wa kujenga maisha endelevu juu ya uovu wa ukatili huo isirudiwe tena .(Barua ya Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili 12 Machi 1998).


Baba Mtakatifu anasitikitishwa na kashfa ambazo hadi leo bado zinajotokeza akisema “kwa bahati mbaya kupambana na kashfa mbaya juu ya wayahudi , tabia hii bado imeenea na inajitokeza kwa aina tofauti kinyume na kanuni za Kikristo katika maoni ya kila mwanadamu anavyo stahili.Kwa mjibu wa Katiba unasema " Kanisa Katoliki inawajibu wa kufanya kila iwezekanavyo na marafiki wote wa kiyahudi kupinga na kupambana  na tabia za ubaguzi na kashfa."

Halikadhalika Baba Mtakatifu Francisko anasema kwamba leo kama ziku zilizopita, mapambano ya kupinga kashfa inawezakana kwa njia ya kuelimisha. Kwa maana hiyo  anawashukuru kwa kazi yao ya kuongeza kampeni za kupinga kashfa kwa njia ya elimu na kuendeleza heshima kwa wote na kuwalinda wadhaifu.Kulinda hazina ya maisha ya binadamu tangu kutungwa kwake hadi mwisho wake wa kuishi.Kulinda heshima ni njia bora ya kuzuia aina zozote za vurugu .Mbele ya janga la fujo ghasia na vurugu zilizotapakaa katika dunia , tunahimizwa zaidi katafuta amani bila vurugu, kwaajili ya kukuza yaliyo mema.


Anamalizia akitoa mfano ya kwamba iwapo tunataka kupalilia magugu ya ubaya, ni dharura ya kupanda yale yaliyo mazuri , kupalilia haki , kuimarisha maelewano, kuunga mkono ushirikiano na siyo kukata tamaa . Kwa nia hiyo tunaweza kuvuna matunda ya amani .Kwa hiyo  ninawatia moyo nikiwa na matumaini ya kwamba kuweka zana muhimu za kuhamasisha utamaduni ambao unathamini kila mahali uhuru wa dini, na kulinda watu wake wa kila dhehebu dhidi ya vurugu na nguvu, pia vyombo vya kuweza kusitisha chuki zisitawale.

 

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.