2017-02-04 14:47:00

Jubilei ya miaka 25 ya Kanisa la Mongolia na tunda la Maparokia


Wapo zaidi ya wamisionari 50 na watawa 14  kutoka nchi tofauti za dunia wanao toa maisha yao katika nchi ya Mongolia, wao ni waaminifu katika wito na kuendeleza uhusiano wa kina na Mungu kwaajili ya kujitoa zaidi kwa jamii na kwa ndugu. Ni kwa huduma hiyo imewezesha Kanisa la Mongolia kujiandaa kuandimisha miaka 25 ya umisionari, ambapo muda si mrefu pia wataweza kufungua parokia tatu.
Padre Prosper Mbumba wa Shirika la Moyo safi wa Bikira Maria kutoka nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC akiongea na Shirika la Habari la Fides wakati wa kuadhimisha sikukuu ya Bwana kutolewa Ekaluni tarehe 2 Februari  sanjari na siku ya watawa duniani kila mwaka  anasema, ni fursa kwao kutafakari wakiwa pamoja na Askofu Mkuu  Wenceslao Selga Padilla Balozi wa kitume wa Papa huko Ulaanbaatar.


Halikadhalika miongoni  mwa watawa wengi waliokusanyika, Sista Nirmala mtawa wa kiindi kutoka katika Shirika la Moyo safi wa Bikira Maria anaeleza juu ya uzoefu wake wa maisha ya kitawa ya kwamba, amefika nchi ya Mongolia miaka zaidi ya 10 na kwamba ni mtawa kwa miaka 18. Sista huyo anakumbuka ya kwamba mwaka jana 2016 Kanisa la Mongolia lilifanya sikukuu kubwa kwa mzaliwa wa kwanza kupata daraja la upadre na kwa mwaka 2017 ni jubileo  ya miaka 25 ya umisionari wa Kanisa baada ya kuondokana na mfumo wa utawala wa kikomunisti.

 

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.