2017-02-03 14:09:00

Wahamiaji haramu ni ukosefu wa kazi katika nchi mahalia


Kodi ya maendeleo ya Ulaya imetenga miradi  kufanya kazi katika nchi zenye kiwango za juu zaidi cha wahamiaji wanaopitia bahari ya meditranea  ili kusimamia utekelezaji wake kwa wahamiaj hao.Ni pendekezo la Katibu mkuu wa Chama cha wafanyakazi (UIL) Carmelo Barabagallo,nchini Italia  wakati wa mkutano wa Kimataifa kwa mara ya kwanza huko Lampedusa kisiwani Italia tarehe 1 Februari 2016 wa kauli mbiu “kwaajili ya bahari ya amani na Kazi”


Kati ya washiriki wa mkutano huo  walio toa hotuba mjumbe kutoka nchi ya Tunisia wa tuzo ya amani kwa mwaka 2015 Hassine Abbassi anasema ukosefu wa ajira pia ni chanzo cha wahamiaji kupita baharini na pia anapinga kile kiitwacho ugaidi unaopangwa , ambapo anasema ndiyo chanzo kikubwa cha wahamiaji, kwani serikali nyingi zimechagua njia za ugaidi kwa madhumuni ya kujitajirisha binafsi, hata kwa gharama ya uharibifu wa nchi nzima.Aidha anasema mapinduzi ya nchi ya Tunisia, yamefanikiwa dhidi ya umasikini  na haki ya kijamii kwa kupata kazi,uhuru na ugawaji  sawa wa utajiri.

 
Na mwakilishi wa kipalestina Husain Fogahaa katika hotuba yake  anakumbusha kwamba ni milioni 6 ya wapalestina wako nchi za ugenini duniani kote na wengi wako katika makambi ya wakimbizi. Anaongeza, japokuwa walikubali Serikali ya Israel , lakini leo hii ni zaidi wa vituo vya ukaguzi 400 vinavyozunguka nchi nzima na kuwanyima haki zao msingi.Anasema “Sisi Wapalestina ni wahamiaji katika nchi yetu." Asilimia 28%ya watu wasio kuwa na ajira na wengi wanaishi katika hali ya umasikini.


Wahamiaji haramu ni vijana wenye umri kati ya miaka 18 na 35 , na wengi  wao ni wahitimu wa elimu ya juu, kama wataalumu wa compututa na sayansi , ni wana uchumi lakini wanakabiliwa na kipeo cha ukosefu wa ajira. Taarifa inaeleza kwamba sababu kubwa ya kiuchumi na ukosefu wa ajira, ukosefu wa kuhama kwa njia halali, na vyombo vya habari kuchochea picha zinazo onesha utajiri wa jamii za Ulaya , ni mojawapo ya sababu msingi zinazosababisha uchaguzi wa wengi kuhama. Hamu ya kusafiri imezidi kuongezeka kwa miaka 25 hivi, na hasa kwa miaka ya karibuni ni vijana wengi wanao kuja katika nchi ya Italia wakifiria kupata msaada.

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.