2017-02-02 15:32:00

Wito wa Maaskofu kwa ajili ya mageuzi katika mfumo wa magereza


Serikali ya Uingereza lazima kuongeza mara mbili jitihada zake za kutekeleza mageuzi gerezani ili kuboresha mfumo wa magereza katika kuokoa maisha ya watu, ni ombi la Maaskofu wa Uingereza na Wales  katika taarifa yao iliyotolewa mara baada ya Wizara ya Sheria na Haki  ya Uingiereza kutoa ripoti juu ya matukio ya wafungwa kujinyonga wenyewe ndani ya magereza.Kwa bahati mbaya ni idadi inayoeleza bayana  juu ya maabusu kwa uamuzi wao wenyewe na visa hivi vinazidi kuongezeka.


Kwa mujibu wa ripoti ni kwamba inaonesha  kwa mwaka 2016 maabusu 119 wamejinyonga wenyewe na kesi 34,784 ni ajali za kujidhuru wao wenyewe na vilevile matukio na vurugu 25,049, hizo ni takwimu za kutisha na hazikubaliki, anasema Askofu Moth Arunde na Brighton wakarugenzi wa makanisa ya wafungwa , wakionesha pia uhaba wa wafanyakazi na msongamano wa wafungwa ambao ndiyo sababu msingi ya uwepo wa matukio kama hayo ndani ya magereza.Pamoja hayo wanaonesha kwamba mwaka jana , kumekuwa na maandamano ya maofisa wa magereza kuhusu afya na usalama kazini , wakati huo wafungwa wengi walionesha kuwa na matatizo makubwa.


Takwimu za sasa juu ya kujinyonga na vitendo binafsi vya kujiumiza wenyewe ndani ya magereza , Askofu Month anasema ni vya kushtua , kwani Kila janga la kifo binafsi ni kuumiza familia yake na wafanyakazi ndani ya magereza wanao jaribu kuzuia vifo hivyo.Kutifia hatua hiyo ya matukio ndani ya magereza , ni jamabo lisilokubalika na anaongeza, inabidi kushughulika kwa haraka masuala yanayohusiana na wafanyakazi na pia msongamano wa wafungwa , na kuhakikisha huduma nzuri na muhimu wafungwa na hata wenye ugonjwa wa akili vinapatikana.


Skofu Arundel na Brighton wanakumbuka  kwamba Mwandishi Dostoyevski , aliandika kwamba "kiwango cha ustaarabu wa jamii unaweza kuhukumiwa kwa kuingia katika moja ya magereza yake ".Kwa nja hiyo ni wajibu wa kila mtu ili kupambana na hali hii.Kwa maana hiyo wito wa  Askofu kwa serikali ni kufanya kwa haraka iwezekanavyo ili mageuzi gerezani yawepo .Kwa upande wa  Kanisa la Uingereza na Wales wanasema kwa pamoja na mapadre wanao hudumia kanisa la magereza na watu wa  kujitolea waendelee na juhudi za kusaidia wafungwa wanaoishi katika mazingira magumu, aidha na kufanya kazi pamoja na taasisi na watu katika vituo vya kizuizi. 

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.