2017-02-02 15:09:00

Fikirieni namna ya kufikia malengo ya kampeni bila vurugu


Tunaomba wanafunzi warudi mashuleni kwaajili ya kuendelea na  mwaka wa masomo wakati huo wakiendelea na kampeni zao halali.Ni maneno ya Maaskofu wa Baraza la maaskofu katoliki wa Afrika ya kusini , kwenye ujumbe ulio tiwa saini na Askofu Mkuu William Salatterry Askofu Mkuu wa Jimbo la Pretoria kwa niaba ya maaskofu wote.
Kwa miezi hii wanafunzi wa Afrika ya kisini wanapinga kuongezeka kwa kiwango cha malipo ya Chuo Kikuu , na maandamamo hayo yamesababisha baadhi ya matukio mengi ya ajali kati yao na nguvu za vyombo serikali.


Kadhalika wanafunzi wanatarajiwa  maandamamo ya kupinga yaanze bada ya ufunguzi wa mwaka wa masomo, na kwa njia hiyo Maaskofu wanaomba kwanza wanafunzi waweze kufikiria namna ya kuweza kufikia malengo ya kampeni zao bila kuvuruga mipango ya  kitaaluma na bila ya kusababisha ghasia.Aidha maaskofu wanatoa ahadi ya kutoa msaada wao kwani wabasema, elimu inapaswa ipatikane kwa watu wote kwa kutegemea usawa na uwepo wa mazungumzo ya upatanisho kati ya sehemu zote mbili, kwamba wanatambua zaidi juhudi na mafanikio yaliyo patikana nchini Afrika ya Kusini katika sekta ya elimu lakini pia wanaomba uwepo wa mwongozo wa uamuzi thabiti kutatua mgogoro huo.

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.