2017-01-26 16:23:00

Chuo cha mafunzo ya madaktari wa watoto huko Bangui


Waliweka Mkataba wa makubaliano wa Hosptali ya watoto Bambin Gesu ,huko  Bangui nchi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati , kwa nia ya kuwaandaa madaktari wapya . Maombi hayo ni mpango thabiti ulio pendekezwa  na Baba Mtakatifu Francisko wakati wa ziara yake ya kichungaji Novemba 2015.
Hayo ni maneno ya Daktari Mariella Enoch Rais wa Hospitali ya watoto  Bambin Gesu Mjini Roma ambaye amepata kusema alipohojiana na mwandishi wa habari wa Radio Vatican, kuhusiana na hospitali hiyo kwamba, alikwenda kutembelea Bangui miezi mitatu iliyopita na kukuta miradi ya Baba Mtakatifu aliyoitamani inaendelea bega kwa bega na kwamba hali ya wakimbizi kwa sasa ni kama inakaribia kuisha.Anasema watu  wanaendelea kurudi katika majumba yao kwa msaada waliopewa.


Na katika ziara hiyo Daktari Enoc anasema walipata kusahini Mradi  wa kwanza wa Hospitali ulio kuwa unatarajiwa , napia kutia sahini  kwa mradi mwingine  na Waziri wa Elimu kwa suala la Chuo Kikuu cha mafunzo ya madaktari   na pia kwa Waziri wa Afya  kwaajili ya kitengo cha maabara ya viungo ambayo inatakiwa iwe pamoja na hospitali  ya watoto huko Bangui.Kwa upande wa Daktari Enoc anasema hicho kilikuwa ni kitendo rasmi ambacho kwasasa  tunawajibika kufanya kazi pamoja na Serikali kwaajili ya nchi.Aidha anasema kwamba pamoja na hayo kuna Mashirika mawili yasiyo  ya kiserikali ndani ya kituo  cha Hospitali ya  watoto ,ambapo kwa wakati huu ni lazima kujaribu kutafuta namna ya kushirikiana kwa pamoja , wamezoea kufanya kazi wao peke yao bilashaka wataweka juhudi zao kuweza kushirikiana kwa pamoja.

Na matumani yetu kwamba sasa  wataanza mapema kukarabati Hospitali ambapo mwezi Septemba pia wataanza kazi  halisi ya Chuo Kikuu cha mafunzo ya madakatari  na hasa watoto, kazi hiyo anasema , watafanya wao kuwafundisha madakatari zaidi wa watoto kutokana kwamba baadhi ya madaktari waliopo hakuna anayeweza kufundisha,kwa njia hiyo daktari anasema itakuwa mafunzo kwa ujumla , watakao ifanya wao, lakini wanayo furaha kuifanya.

Daktari Enoc anasema  jinsi ilivyo anza mradi huo kwamba,  wazo lilitokana mara baada ya Ziara ya Baba Mtakatifu  huko Jamhuri ya Afrika ya Kati, yeye Mwenyewe aliwaoomba wakuu wa Hosptali hiyo aweze kuisiamia, mara baada ya kuitembelea na kuona hali halisi ilvyokuwa ngumu .Baada ya kurudi Roma  alimwita Daktari Mariella kwa mkutano na kumuona ashughulikie mradi huo kati ya miradi ya hosptali.


Jambo la kufurahisha  anasema Daktari ni kwamba wao wanafanya kazi kwa ushirikiano na chi na siyo kufanya kazi kwaajili ya nchi. Kwa njia hiyo na kweli juhudi kubwa ya kushirikishana na mamlaka ya nchi ambao ndiyo wanao wajibu wa huu ili kuifanya nchi iweze kukua ndani yake.Paomja na hayo Dkarari anasema inahitaji juhudi kubwa  ya kufanya hospitali mpya na uendeshaji wake iwapo kuna utashi , pia anafikiri Daktari Enoc ya kwamba ni sawa na mawazo ya Baba Mtakatifu asemayo kwamba  ni kusaidia ukuaji kwa ujumla wa nchi.Licha ya miradi hiyo kuna hata mradi mradi mwingine wa kilimo ulio kabidhiwa  katika Shirika la Wakarmeli huko Bangui ya kwamba , ni mradi muhimu kwasababu baada ya kuwakabidhi nyumba , kinachofuata ni kuanza kuwapa kazi na wakati huo huo afya, na hii Daktari anasema ni kama vile Baba Mtakatifu aliweza kuchukua kwa ujumla nchi yote.Lakini kwa dhati naweza kusema , mabadiliko yanaonekana  kwa miezi miwili tu. 

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.