2017-01-24 17:14:00

Wawakilishi kutoka Baraza la Kipapa kutembelea Aleppo


Mwakilishi wa Papa  katika Baraza la kipapa la maendeleo endelevu ya Binadamu  Askofu  Giampiero Dal Toso alikwenda kutembelea Aleppo akiwa na Kardinali Mario Zenari ,Balozi wa Kitume huko Syiria na Mons Thomas Habib  Kuanzia tarehe 18 -23 Januari 2017.Hiyo ilikuwa  ni ziara ya kwanza maalumu kwa wawakilishi wa Vatican inapolekea kumalika kwa  vita ya Aleppo.Wawakilishi hao walipata kukutana na jumuiya za kikristo na wachungaji wao, ambao walimshukuru Baba Mtakatifu Francisko , kwa juhudi zake za kuhamasisha misaada ya  Syiria. Pamoja na hayo waliwatembelea Taasisi Katoliki na pia makambi ya wakimbizi.


Kwa namna ya pekee walifanya uzinduzi wa chombo cha kibinadamu kinachoendeshwa na Caritas ya Aleppo katika mtaa wa Hanno.Wakati wa ziara hiyo pia walifanya  sala na maombi ya kiekumeni  kwaajili ya tukio la wiki ya maombi ya umoja wa wakristo inayoendelea  , na walijionea hali halisi ya uharibifu wa  vituo vya afya katoliki , ambapo kwa mwanga zaidi vinaweza kukarabitiwa  na vikaweza kufanya kazi.
Licha ya hayo walifanya mkutano pia na wawakilishi wa dini ya kiislam na wote walisistiza jukumu la kuelimisha dini , amani na maridhiano.Wakati wa ziara hiyo pia  viongozi wa nchi na madhehebu walitoa pongezi  kubwa kwa Baba Mtakatifu Francisko ,kumteua Kardinali mpya kutoka katika nchi yao na kusema hiyo ina maana ya kutambua  ukaribu zaidi wa papa na watu wa Syria.


Katika mikutano  na Tasisi za kutoa huduma katoliki  waliona  umuhimu wa msaada unaotolewa kwa manufaa ya watu wa Syiria. Kwa msaada  wa Kanisa zima la Ulimwengu na juhudi kutoka katika jumuiya  za kimataifa , na msaada  huo unaweza kuimarisha  na kujenga wakati ujao na kukidhi mahitaji mbele ya ongezeko la watu .Miongoni mwa dharura hizo , kuna haja na kuangalia hasa vitu vinavyohusiana na mahitaji muhimu kama chakula  mavazi , elimu , afya na makazi .

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.