2017-01-24 16:37:00

Kufanya mapenzi ya Mungu si kwamba hukasiriki na Bwana


Kufanya mapenzi ya Mungu haimanishi  usibishane au kumkasirikia Bwana , la muhimu uwe mkweli na iswe mnafiki na mwishowe ukamwambie “tazama mimi hapa”,ni maneno ambayo yamejitokeza katika mahubiri ya Baba Mtakatifu Jumanne 24 Januari 2017 wakati wa Misa Takatifu katika Kikanisa cha Mtakatifu Martha Mjini Vatican . 
Kiini cha mahubiri ya baba Mtakatifu Francisko ni kutoka katika barua ya Wahebrania  iliyosomwa ya siku “wakati Kristo alipokuja duniani, wewe hukupendezwa na dhabihu na sadaka ya kuteketezwa na kuondoa dhambi. Tazama mimi ninakuja kufanya mapenzi yako”. Hili neno la Yesu alisema Baba Mtakatifu , linafunga historia  ya “tazama mimi hapa “maana yake ni historia ya wokovu .Baada ya Adamu aliyekuwa mafichoni kwasababubu ya hofu ya Bwana , Mungu alianza kumwita , na akasikia sauti ya mmojawapo walio kuwa wamejificha ikiitikia  “mimi hapa “maana yake “niko tayari”. Tazama mimi ni kuitikia kwa Ibrahimu, Musa, Eliya, Isaya , Yeremia hadi kufikia  mimi hapa ya Maria ambayo  ilikuwa ya mwisho  wakati wa kuchukua mimba Yesu. Ni historia ya tazama mimi hapa  lakini siyo ya moja kwa moja kwasababu  Mungu anazungumza na wale anao karibisha.


Baba Mtakatifu anaendelea kuelezea kwamba,  Bwana anaongea na wale anaowakaribisha  ili waweze kutembea katika mwelekeo huo “tazama mimi hapa. Yeye ana uvumilivu mkubwa , kwani tunaposoma katika kitabu ya Ayubu, maneno na tafakari ya Ayubu ambaye hakuelewa na wala kujua majibu , ambayo Bwana alimwambia na kumkosoa, Lakini  mwishowe ile ndiyo ya Ayubu  kwa Bwana na kusema  wewe una haki,kwani mimi nilikujua tu kwa kusikia tetesi, na sasa macho yangu yanakuona wewe .Ni kusema ndiyo  wakati ukiwa na utashi , kwani maisha ya kikristo ndiyo hayo ya kusema tazama  mimi hapa” kuendelea kufanya mapenzi yako Bwana. Ni vizuri kuendelea kusoma neno katoka  katika Biblia Takatifu na kujaribu kutafuta majibu ya watu  wanao itikia wito kwa Bwana, na kwa kupata jibu hilo ni jambo zuri sana , Baba Mtakatifu  alisema na kuongeza, mimi hapa niko tayari kufanyua mapenzi yako.
Baba Mtakatifu Francisko anatoa maswali mengi akitumia mifano kutoka katika Biblia Takatifu akisema:Je Ninakwenda kujificha kama Adamu ili ni sijibu? Au wakati Bwana akiita , badala ya kusema mimi hapa , au unataka nini kwangu? Ninatoroka  kama Yona ambaye hakutaka kufanya kile alichatakiwa na Bwana? Au ninafanya makusudi kufanya Mapenzi ya Bwana  kwa mtazamo wa kijuu juu tu , kama wale walimu wa sheria, ambao Yesu aliwahukumu vibaya , kwani walikuwa wanafiki.Baba Mtakatifu anasema , kila kitu sawa , hakuna maswali,na wala mimi sifanyi chochote zaidi au ninangali njia nyingine kama walivyo fanya Mlawi na Kuhani mbele ya mtu masikini aliyejeruhiwa , na kupigwa na majambzai , akaachwa nusu ya kufa. Jibu langu kwa Bwana ni lipi?


Aidha Baba Mtakatifu Francisko anasema : Bwana  anapenda kubisha na sisi, akitoa mfano juu ya hilo anafafanua na kusema, mtu anasema , Mimi Padre , mara nyingi ninapokweda kusali ninapata hasira na Bwana, lakini hata hiyo ni sala, Baba Mtakatifu anasisitiza na kuongeza, Yeye kwani anapenda anapoona kwamba umekasirika na unamwambia yeye uso kwa uso kile ambacho unajisikia, kwasababu yeye ni Baba! Na hiyo pia ni jibu la “mimi hapa. Alimalizia akisema akiuliza pia  je mimi ninajificha , au ninajifanya manafiki, au ninaangalia mahali pengine?Kila mmoja wetu wetu anaweza kujibu  jinsi gani mimi ninaitikia ndiyo mimi hapa , tayari kufanya mapenzi ya Bwana katika maisha yangu. Na Roho Mtakatifu atupatie neema hiyo ya kupata jibu.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili, ya Radio Vatican 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.