2017-01-20 14:03:00

Tuwape mshikamano wetu na msaada wakazi wa nchi Takatifu


Ujumbe kutoka  kwa Maaaskofu wa shirikisho la makanisa Katoliki ya Ulaya , Marekani na Afrika ya Kusini baada ya hija yao ya mshikamano katika nchi Takatifu kuanzia 14-19 Januari 2017, hija ya mwaka huu imewakilishwa na maaskofu 12.
Ujumbe unasema watu wengi katika nchi Takatifu wameishi maisha yao yote  chini ya utawala na ubaguzi wake , mgawanyiko wa kijamii  lakini pamoja na hayo bado wanaendelea kukiri imani yao kwa matumaini na mapambano kwaajili ya maridhiano.Kwa njia hiyo hawa wanastahili leo na  daima mshikamano wetu. Wajibu wao Maaskofu  ni ule wa  kuondoa ujenzi wa kuta katika makazi ambayo ni ukiukwaji wa haki za wapelestina kwenye maeneo kama vile Hebron na Yerusalem ya mashariki pamoja na kwamba  imetambuliwa na Umoja wa mataifa hivi karibuni na kusema kuwa kuna hali ya hatari  ya ukosefu wa amani.


Hata hivyo uwajibikaji ni kutoa misaada kwa wakazi wa Gaza ambao wanaendelea kuishi katika majanga ya kibinadamu yaliyotokana na binadamu mwenyewe , kwa miaka mingi wakiishi kwa kuzingirwa pande zote na hasa uadui wa kisiasa uliosabishwa na ukosefu wa nia njema ya pande zote zinazohusika .Kama Baba Mtakatifu Francisko anavyotukumbusha ya kwamba watu wote tunapaswa kuwajibika ,kwa kuwatia motia moyo, katika kuhamasisha kupinga vurugu  ambayo imeleta   mabadiliko makubwa ulimwenguni . Kwa maana ya kwamba kuna ulazima wa kuwajibika mbele ua ukiukwaji wa haki msingi  kama vile ujenzi wa kuta  za kutengenisha Palestina  ikiwa pamoja  na Bonde la Cremisan.


Wote kwa pamoja tunao wajibu wa kuhamasisha kwa kutafuta  suluhisho  kati nchi mbili .Vatican ilisistitiza ya kwamba iwapo nchi ya Israel na Palestina hawatakubali kushikana bega kwa bega , maridhiano kati ya  viongozi wa ndani ya mipaka iliyo afikiana  na kujulikana  kimataifa, amani hiyo itabaki kama ndoto ya mbali na pia usalama usio kuwa na uhakika. Wote pamoja tunao wajibuwa kusaidia Kanisa mahalia  katika mahitaji yake kama vile Taasisi mbalimbali, mashirika yasiyo ya kiserikali, valantia, kwasababu  katika hali ngumu sana  vyombo hivi vimeonesha  ujasiri mkubwa katika kazi yao inayobadili maisha.Imani yetu kwa Mungu inatupa matumaini,pamoja na ushuhuda wa wakristo wa Nchi Takatifu tulio kutana nao na hasa vijana na watoto wametuhamasisha kufanya hivyo.
Ujumbe wao unamalizia kwa kusema , Biblia inatuambia hivi: “mwaka wa hamsini mtauheshimu kwa kutangaza uhuru kwa watumwa , (Walawi 25:10).Kwa kipindi cha miaka 50 ya kutawaliwa , ni lazima kuwaombea watu wapate uhuru wa kila mtu katika nchi Takatifu na kuwapatia msaada wa vitendo na kufanya kazi kwa ajili ya mani na haki. 

 

Waliodhuria hija Takatifu ni  Askofu wa  Declan Lang, Uingereza na Galles (Rais wa kamati ya maandalizi ya Hija nchi Takatifu),Askofu Stephen Ackermann, Ujermani, Askofu Peter Burcher, kutoka Mabaraza ya maaskofu wa nchi za Kaskazini mwa Ulaya. Askofu Oscar Cantú, Marekani, Askofu Christopher Chessun, Kanisa la Uingereza , Askofu Michel Dubost, Ufaransa, Askofu Lionel Gendron, Canada; Askofu Felix Gmür, Uswis,Askofu Nicholas Hudson, Kamati ya Mabaraza ya maaskofu wa shirikisho la Ulaya,Askofu William Kenney, Uingereza na Galles; Askofu William Nolan, Scotland .Wakisaidiwa na Munsinyo Duarte da Cunha, Baraza la maaskofu wa Ulaya na Padre  Peter-John Pearson, Baraza la maaskofu wa Afrika ya Kusini.

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.