Ni zaidi ya mwaka mmoja umepita bila kuwa na taarifa za Padre Gabriel Oyaka,
mwanashirika wa wa Shirika la Roho Mtakatifu huko Nigeria , aliyetekwa nyara 7 Septemba
2015 huko Kogi .
Akiongea na Waandishi wa habari mara baada ya misa ya kumbukumbu ya Padre aliyetekwa,
Cardinali Olorufemi Onaiyekan, Askofu Mkuu wa Abuja, alikumbuka kwamba wateka nyara
hawakusikika au kufanya mawasiliano ya kutaka malipo ya fidia,hivyo ni juu ya mamlaka
ya serikali kuwajibika kulinda maisha na mali za raia wa Nigeria na Kanisa haliwezi
kufanya chochote zaidi ya kuiomba serikali kufanya kazi yake.
Aidha akizungumzia juu ya matukio kadhaa ya utekeji wa wazalendo wasio kuwa na hatia
, wakiwemo kati yao mapadre, Kardinali Onayeiyekan anabainisha kuwa “majanga haya
yameandama nchi yetu, na jina lilaosikika sana ni wafugaji wa kabila la Fulani ambao
wamekuwa wakijihusisha na mahuaji, utekaji,na uhalirifu wa maisha na mali zao”
Wafugaji wa kabila la Fulani wameshitakiwa mara nyingi kwa kushambulia vijiji kadhaa
vya wakulima kwasababu ya hoja zao ya kuhamahama wakitafuta malisho mapya ya mifugo
yao.kwahiyo Kardinali alihitimisha akisema "kwa mtazamo wangu, tunakabiliwa na dharura
ya janga la Kitaifa na kwa nchi nzima lazima kuungana pamoja kukomesha vurugu hizi.
Sr Amgela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |