2017-01-19 15:10:00

Historia ya Ukristo Ulaya imepitia kipindi kigumu tufanye kumbukumbu


Wakristo wa sehemu zote za dunia wameanza sala ya kuombea  umoja wa wakristo  ulionza Jumatano 18 Januari na unatrajiwa kumalizika tarehe 25, januari 2017 katika kilele cha sikukuu ya kongoka kwa Mtakatifu Paulo Mtume na mwalimu wa Mataifa .
Maombi hayo kwa mwaka 2017 yameongozwa  Kauli mbiu Upanisho: Upendo wa Kristo unatuwajibisha ambapo viongozi wa wakuu wa Makanisa katoliki ya Umoja wa Ulaya wametoa ujumbe kutokana na tukio hili wakisema hakika maneno ya Mtakatifu Paulo kwa wakorinto yanatuhamasisha kusali kwaajili ya umoja wa wakristo.


Katika ujumbe wao wanasema historia ya Ukristo Ulaya imepitia katika kipindi kigumu kilichosabisha mgawanyiko na hata  hukumu na kutumia  nguvu.
Aidha wanasema tukio la maombi ya sala kwa mwaka huu  limeangukia wakati baadhi ya makanisa wanajiandaa kusheherekea maadhimisho ya miaka ya 500 ya mageuzi na mwanzo wa kiprotestanti.Tunapenda kukumbuka  tena kipindi kigumu cha siku zilizopita  kwa sababu kufanya kumbukumbu ya matukio na kukabiliana historia yetu ni fursa ya pekee yenye thamani  katika kurudia kwa  upya wajibu wetu wa kuponya majeraha na kushinda mgawanyiko huo.


Na kwa  hiyo  tuelekeze mioyo yetu kwa Yesu Kristo, ambaye ni mpatanishi wa watu wote na muumba na Mungu , ili atuongoze katika  kutekeleza wajibu huo.Ni kwa njia ya unyenyekevupia shukrani tulizopewa tufanye mapatano kwa njia ya maneno na matendo yetu.Leo hii tunaadhimisha tulivyo komaa na kujifunza kushirikiana kazi kwa pamoja, juu ya mazungumzo taalimungu.Aidha ujumbe unasema; Viongozi wakuu  wa Mabaraza ya Maaskofu Katoliki wa Ulaya, tumekuwa tukishirikiana kwa miaka 45 kwa pamoja katika masuala kadhaa yenye maslahi ya pamoja,ni pamoja na kushirikishana mateso na furaha za dunia inayotuunganisha.


Ujumbe unataja baadhi ya shughuli za pamoja ;mshikamano wetu na watu wote ,hata watu wasio kuwa na kabila (ROM), juhudi zetu kwa upande wa haki na amani na mazingira, maombi kwa anjil ya umoja wa ndani katika mwilisho wa Kristo ,ni mambo yaliyo tutia nguvu katika mahusiano yetu.
Pamoja na yote zipo hata changamoto wakisema, migogoro mingi ambayo Ulaya na nchi za jirani tumeitwa kukabiliana , ni muhimu zaidi kwani  vita, na migogoro , kutokuwa na uhakika wa kisiasa , uhamiaji na changamoto ya mazingiria, umasikini wa mali na wa kiroho, vina athiri maisha ya kila mtu katika nchi za Ulaya na kwingineko lakini pamoja na  migogoro hii yapo  pia matumaini. Kwa njia hiyo  tunaweza kushuhudia upendo wa Kristo kwa maridhiano kupitia uadilifu na kazi ya uumbaji ,  mshikamano dhidi ya  maskini na ulinzi wa heshima ya watu wa Mungu.


Hitimisho la  ujumbe; kwa upande wetu tunapaswa kuimarisha zaidi njia ya mazingumzo kwa pande zote. Kwa njia ya  shuhuda na matendo tujenge madaraja, kwa njia ya  maombi tujifunze  kutambua kazi ya Roho Mtakatifu .Njia ya kufuata yawezekana kuonekana ni rahisi, lakini cha  muhimu ni kukazia  ukweli wa maneno haya ya “upendo wa Kristo unatuwajibisha”.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.