2017-01-18 14:38:00

Mashahidi wa Uganda 2017 kuongozwa na kauli mbiu "kuweni imara katika imani"


Katika kuadhimisha sikukuu ya mashahidi wa Uganda kila ifikapo tarehe 3 Juni ya Kila mwaka, Kwa mwaka 2017 Baraza la Maaskofu wa Uganda wamechagua kauli mbiu itakayoongoza siku hiyo kwamba “ kuweni imara katika imani kama  mlivyofundishwa.” Aliyatamka hayo Askofu Vincent Kirabo wa Jimbo la Hoima kwa siku zilizopita kwamba  kauli hiyo imechaguliwa kutoka  katika Barua ya Mtakatifu Paulo kwa  Wakolosai  (Kol 2,7)
Muhusika wa maandalizi ya tukio Emmanuel Kiiza Aliba alisema ;kauli mbiu hiyo inajikita katika ushuhuda mkubwa  kwa waamini wanao paswa kuutoa kwa Kristo, mtu binafsi,  katika familia, katika maeneo ya kazi na kwa sehemu zozote ambazo tunakuwapo. Pamoja na hayo katika sikukuu ya mashahidi wa Uganda itakuwa na maana kubwa kwa  Jimbo la Hoima kutokana na kwamba mwaka jana 2016 Jimbo lilisherehekea miaka 100 ya uinjilishaji na kwa mwaka huu wanategemea kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 52 ya kuundwa kwa jimbo. Aliongeza Aliba tumekomaa kiimani , na sasa tunapaswa kutafakari kwa kina Injili.

 
Kwa kawaida sikukuu ya Mashahidi wa Uganda , ufanyika kila tarehe tatu ya mwezi wa sita, na sherehe hizo ufanyika katika Madhabau ya mashahidi Namugongo, kwa njia hiyo  maandalizi ya mwaka huu yanatarajiwa kuanza na sala ya Novena.Mashahidi wa uganda kwa ujumla ni 45 wakiwa ni wakatoliki na wangilikani.
Mfiadini wa kwanza anayejulikana sana ni Mtakatifu Carol Lwanga,kwani  yeye na wenzake waliuwawa kinyama  kwa kutetea imani yao chini ya utawala wa kifalme wa Mwanga (1884-1903);Na kifo chao kilitokea  kati ya Novemba 1885 - 27 Januari 1887. Tarehe 6 Juni 1929 walitangazwa kuwa wenye heri na Baba Mtakatifu Benedikto wa XV; na tarehe 8 Oktoba 1964 wakatangazwa watakatifu na Baba Mtakatifu Paulo VI.


Ikumbukwe Novemba 2015 katika safari yake ya kitume  huko Afrika , Baba Mtakatifu Francisko alielekea katika madhabahu ya Namungongo Uganda , wakati wa mahubiri yake alisema  kwamba kurithi mashahidi wa Uganda, ni kurithi maisha yaliyo ongozwa na nguvu ya roho Mtakatifu na kwamba ni maisha yanayo toa ushuhuda hata sasa katika kuleta  nguvu ya mageuzi ya  Injili ya Yesu Kristo.
Halikadhalika alisema; ”hatuwezi kutunza urithi huu kuwa kumbukumbu ya kawada au kuhifadhi hiyo kumbukumbu katika jumba la  makumbusho kama kito cha thamani, bali tuna heshimu kweli, na kuwaheshimu watakatifu wote,na zaidi ni kuleta ushuhuda wao wa  Kristo katika nyumba zetu, kwa jirani zetu, katika sehemu za kazi , na katika vyama vya kijamii,ushuhuda huu uwe katika nyumba zetu, na hata mahali popote tutakapo kwenda  pembe za dunia.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.