2017-01-17 15:20:00

Mazungumzo yawe ya amani badala ya uchochezi wa kuleta vurugu


Katika siku ya wiki ya 12 ya sala kwaajili ya amani , ifanyikayo kila mwaka jimbo Kuu la  Gulu Uganda ,Askofu Mkuu John Baptist Odama na Rais wa Baraza la Maaksofu Uganda , alitoa wito kwa watu wote juu ya kuhamasisha amani badala ya wale wanatetea virugu . Aliwakaribisha watu wote waweze kufanya mazungumzo ya amani   badala ya maongezi ya uchochezi kwasababu ya  kusaidiana kuleta amani kwa wote.Gazeti la Fides limemnukuu akisema, "naomba kila moyo usiwaze vurugu, wala kuchochea vurugu na kadhalika kila juhudu za mwili zisihamasishe vurugu".


Makutano hayo ya sala yalianza tarehe 9 -13 Januari 2017  Mahujaji wa amani  zaidi ya elfu tano walipata kuudhuria kutoka pande za kaskazini mwa Uganda, kusini mwa Sudan,na pia wengine kutoka jimbo kuu la Gulu katika  majimbo ya Nebbi , Arua na Lira.Kauli mbiu ya siku hiyo ilikuwa  kama ya Baba Mtakatifu Francisko aliyoichagua katika sala ya amani kwa dunia nzima kwa mwaka huu 2017 yasemayo "Kutokutumia nguvu: mtindo wa siasa ya amani”; ambapo anawaalika  binadamu wote kutokutumia nguvu na kuhamasisha amani. 

Monsinyo Odama aliwageukia kwa namna ya pekee mahujaji , akiwataka wasali kwa ajili ya nchi na kwa ulimwengu , ambapo bado kuna migogoro ya kivita ,kama vile Sudan ya Kusini, Somalia, Afghanistan, Syria, Iraq, Mali, Libya, Yemen, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) , Jamhuri ya Afrika ya Kati (RCA), Nigeria, Gambia na Uganda.Aidha Askofu Mkuu aliwataka viongozi wote wa dini kuzingatia suala la amani ambapo yeye mwenyewe amekuwa na  jukumu muhimu katika hitimisho la miaka  ishirini  ya vita kati ya vikosi vya serikali , na chama cha upinzani (LRA) Kaskazini mwa Uganda. 

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.