2017-01-16 15:02:00

Upatanishi wa watu ni Kanisa kuwa karibu yao kwa ajili ya amani


Changamoto, fursa zaidi, na zaidi ya yote  ni ushuhuda wa ukaribu wa Kanisa kwa watu. Hiyo ndiyo ilikuwa kazi ya upatanishi uliyofanywa wiki za hivi karibuni katika nchi ya  Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Hayo yalisema na Askofu Nicolas Djomo Tshumbe  Rais wa Zamani wa Baraza la Maaskofu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo alipohojiwa na Gazeti la Osservatore Romano, kuelezea namna ya Kanisa likmukuwa kati yao katika kuelekea uchaguzi mkuu nchini humo.
Anasema kwamba wakati  wakuu walifanya mkutano wao huko Angola mwaka jana Oktaba 2016 kwenye Mkutano ulioitishwa na mkutano wa Kimataifa wa kanda ya maziwa  Makuu, Umoja wa Mataifa, na mashirika mengine ya mikoa, wali mshauri Rais  Joseph kabila , kuteua wapatanishi kutoka Baraza la maaskofu , kwa kuzingatia ushawishi wa Kanisa , uhusiano  wake na wadau wa kisiasa , na zaidi ya yote uwepo wake katika kijikita kwenye masuala   msingi ya jamii.


Kwa jinsi hiyo nasema "tuliweza kuzingatia na kufanya mazungumzo kwa pande zote mbili zenye migogoro: sehemu ya mashirika ya  kiraia na sehemu ndogo ya wapinzani, na wengine wengi walio katika upande wa Rais". Aliendelea; “tulikutana kwenye wiki za hivi karibuni kwa pamoja na wadau wa sera zote za  kisiasa: wanachama wa upinzani,na wale kwa upande wa Rais;kutokana na kuamini Kanisa, wote walipata kuitikia wito wetu , na kujadili kwa wiki tatu katika maelewano ya kisiasa, hadi kufikia makubaliano ambayo yataruhusu sera zote mbili za siasa kutawala nchi pamoja mpaka uchaguzi ujao.Aidha anasema pamoja na hayo yote kuna kipengele kilicho muhimu sana  cha makubalianao ya kwamba Rais Kabila hataweza kugombea kwa hawamu ya tatu bali ataendelea kutekeleza majukumu yake hadi uchaguzi ujao,kwa dhana kwamba ni kuhakikisha ,unakuwepo mwendelezo wa serikali kwani  katiba ya nchi inaruhusu. Hata hivyo Kabila alijitahidi kutokufanya marekebisho ya katiba,kuhusu  kura za maoni au utaratibu wa bunge wala wakati wa kipindi cha usimamizi shirikishi. Hii imepunguza mvutano kati ya idadi ya watu  na kurejea kwa matumaini dhidi ya mabishano makubwa ya kisiasa.Hiyo ni hatua muhimu ya makubaliano, kwa wakati wa wiki hizi ambapo tuko katika  kazi juu ya sheria utekelezaji.

 

Kuhusu majadiliano yao ya kikao hicho Askofu anasema kwamba : katika hatua hizo za muda , inahusu kufanya majadiliano ya Waziri mkuu , ambaye anapaswa kuwa msimazii wapande zote za upinzani, kuzungumzia juu ya ukubwa wa Serikali ambayo ataingoza kuelekea uchaguzi.Inabidi kufikia uamuzi katika ya mgawanyiko uliopo na majukumu kati ya vyama.Aidha anabainisha kwamba inabidi kuzungumza katika Baraza la taifa kwa  kufuatilia makubaliano, mengine ni kusubiri muda itakapofika uteuzi wa Waziri mkuu , wakati serikali itakapopitisha bunge. Akaongeza kwamba walichokifanya ni kuwaomba wapate ufumbuzi wa haraka iwezekanavyo .”Tunapaswa kufikia makubaliano haraka iwezekanavyo”.

 

Aidha alisema, kwamba anamshukuru Baba Mtakatifu Francisko , kwa sababu yeye amesaidia wao tangu mwanzo . Kwani tarehe 19 Desemba mwaka jana ,walikutana na baraza la maaskofu wa Congo na waliwatia moyo katika kazi ngumu wanayo kabiliana nayo.Kwa hali halisi kweli bado hali ni teta sana , kwani hata vikosi hivyo vya kisasa vinatuomba tuendelee kuwasindikiza katika mchakato wa kisiasa.Inabidi kuandaa hadi kufikia uchaguzi pamoja na matatizo yote yatakayojitokeza.Kama nilivyokwisha kusema, kwamba sekta za wanasiasa , wametuomba kwa matumaini tuwasindikiezikize na hili kwetu ni fursa ya kweli na inayoleta matumaini.


Afrika inaweza kuondoka na migogoro kwa wakati ujao? Askofu anasema , migogoro inaletwa na sababu mbalimbali. Katika ukanda wa Maziwa Makuu, mara nyingi ni sababu za kiuchumi na katika nchi yetu,Lakini sababu nyingi zinajihusishwa na kunyonywa kwaajili ya madini ,hasa katika ukusanyaji wa madini muhimu  yenye thamani yenye kutengeneza wa Kompiuta.Ni lazima kulenga sera za wanasiasa wakawa na moyo wa kujikita zaidi katika  maslahi ya pamoja na siyo tu ya binafsi, na hiyo inawezekana kwa njia ya kuelimshwa. Ni lazima kuwa na wanasiasa waaminifu na wenye uwezo  wa kufanya kazi kwa ajili ya nchi yao na jamii zao na si kwa ajili ya manufaa binafsi. Hiyo ndiyo njia pekee ya kufikia hali halisi ya sheria. Na kwa namna hiyo tunaweza kupata mfumo ambao ni wa kulinda watu walio dhaifu na wanaoishi katika mazingira magumu, hasa wanawake na watoto. Kwa kifupi, ingekuwa vizuri kufuata mafundisho ya kijamii ya Kanisa, na kwa pamoja tukafanya  kazi katika mwelekeo huu kwa ajili ya baadaye na kujenga jamii mpya ya Congo.

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.