2017-01-16 09:31:00

Tugundue njia rahisi ya kufikia utandawazi chanya usio na utofauti


Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi tarehe 14 Januari 2017 amekutana na wajumbe wa "Global Foundation na kutoa hotuba yake akisema , anayo furaha kwaajili  ya meza yao ya mduara ya chama hicho cha " Roma Global Foundation", ikiongozwa na kauli mbiu inayaofanana na chama chao “kwa pamoja tujibidishe kwa manufaa ya ulimwengu” ili kuweza kugundua njia rahisi ya  kuweza kuwafikisha kwenye utandawazi wenye muungano chanya,tofauti na utandawazi wenye utofauti.Nia kubwa ni kuhakikisha  kwamba jumuia zote zilizoundwa, taasisi,na mashirika katika jamii waweze kufikia malengo ya kimataifa yaliyo kubaliwa kwenye ajenda ya 2010 ya maendeleo endelevu

Baba Mtakatifu anasisitiza kuwa kuna aina ya mifumo  isiyokubalika , mifumo ya kiuchumi ambayo inatupilia mbali  watu kwa  kwa madai ya kwamba hawa hawaonekani,na hata kuleta faida kulingana na vigezo vya faida ya makampuni au mashirika mengine.Tofauti hizo husababisha wengine kunyimwa haki msingi za kiutu hasa katika mifumo ya kisiasa na kiucumi.Wale wenye kusababisha au kuruhusu tofauti ya wengine hawajali  wakimbizi, unyanyasaji wa watoto, maskini wanao kufa kwenye  mitaa na barabarani wakati  wa baridi .Hata hivyo Baba mtakatifu Francisko anasema  wanao sababisha hayo ugeuka kuwa kama mashine zisizo kuwa na roho  kwa kukubali kanuni hiyo lakini  mapema au baaye, hata wao watakuja kubaguliwa watakapokuwa hawana manufaa tena katika  jamii ambayo iliwazesha kuweka kipaumbele fedha zao.

Mwaka 1991, Mtakatifu John Paul II, wakati wa kuanguka kwa mfumo wa ukandamizaji wa kisiasa na kutokea maendeleo ya ushirikiano wa taratibu za masoko  ambayo tunaweza kusema  ni ya utandawazi, alihisi hatari ambayo ingeenea popote na hasa itikadi za kiuchumi.Kwani hizo  zingesababisha kidogo au bila kujali matukio ya kubaguliwa , unyonyaji na kutengwa kwa binadamu, na kupuuza wengi wanao ishi katika hali ya umasikini unaokithiri, unyanyaso, na upofu wa kuwakabidhi suluhisho pekee kwa maendeleo katika  nguvu za masoko.

Kwa bahati mbaya , hatari aliyo kuwa ameona Mtakatifu Yohane Paulo II kwa kiasi kikubwa imejitokeza.Pamoja na hayo yote lakini,zimejitokeza juhudi za maendeleo  kutoka kwa watu binafsi na taasisi ya kutuliza tahabu, ubaya na mateso yaliyo tokana na utandawazi usio wajibika. Alitoa mfano wa juhudi hizo kwa ushuhuda wa Mama Teresa wa Kalcutta , ambaye yeye mwenyewe alipata furaha ya kumtanganza Mtakatifu  miezi michache iliyopita na mbaye ni ishara  ya nyakati zetu, kwa namna fulani, aliwakilisha jitihada hizo.Baba Mtakatifu Francisko anasema yeye aliinama na kuokoa watu walio kuwa wameachwa pembezoni mwa barabara wakiangaika au kufa, kwa kutambua kila mmoja utu wake aliopewa na Mungu. 

“Yeye alikaribisha maisha ya kila mwanadamu, ambaye hajazaliwa ,  na yeye aliyekuwa ametupwa kwenye takataka, aidha, yeye alifanya asikike sauti yake kwa watawala  wa nchi, ili wapate kujua uhalifu  na umasikini ulio sababishwa na wao wenyewe”.( Mhubiri ya Baba Mtakatifu kwa tukio la kutangazwa  mama Teresa wa Kalcutta 4 Septemba 2016)
    
Baba Mtakatifu Francisko anasema hii ni tabia ya kwanza ambayo inaweza kusababisha utandawazi wa mshikamano na vyama vya ushirika. Ni muhimu, hawali ya yote kwamba kila mtu, binafsi,  asiwe tofauti na majeraha ya masikini, bali ajijfunze kuteseka na wale ambao wanakabiliwa na mateso, upweke, kukimbia kwa kulazimishwa au kutengwa na familia zao; pamoja na wale ambao hawapati huduma za afya pamoja na wale wenye njaa na baridi au joto.
Huruma hii itahakikisha kwamba wanaondesha sera za kisiasa na kiuchumi wanaweza kutumia akili na pia rasilimali zao siyo tu kuthibiti na kufuatilia athari za utandawazi, bali wapate kusaidiwa kwa njia ya sekta mbalimbali za kisiasa , mikoa , taifa na kimataifa, kuwasahihisha kwa kuwapa mwongozo kila inapobidi.Baba Mtakatifu aliongeza ; Siasa na uchumi, kwa hakika  wanapaswa kutambua zoezi hili la wema na busara. 

 

Kanisa daima  lina amini, Baba Mtakatifu Francisko  anasema  kwasababu linajua uwezo mkubwa wa akili ya binadamu ambaye daima ukubali asaidiwe na kuongozwa na Mungu,na hata utashi mwema walio nao wadogo na wakubwa kama vile masikini , matajiri, waajiri na wafanyakazi.Wito wake baba Mtakatifu ni kuwatia moyo waendele na  ahadi yao inayoongozwa daima na mafundisho ya Kanisa, wakihamasisha ule utandawazi katika vyama vya pamoja na wadau  wote husika kama vile , vyama vya kiraia, serikali, mashirika ya kimataifa, kitaaluma,kisayansi jamii na wengine . Alimazia hotuba yake  akiwatakia matashi mema ya kazi zao.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.