2017-01-13 16:05:00

Vikosi vya ulinzi na usalama: Hapa ni kazi na sala!


Baba Mtakatifu Francisko, Ijumaa tarehe 13 Januari 2017 amekutana  na vikosi vya ulinzi na usalama vinavtoa huduma yake mjini Vatican ili kutakiana kwa salamu na matashi mema ya mwaka mpya wa 2017 kama ilivyo  utamaduni wao  wa kukutana nao kila mwaka. Akianza na salamu  kwa niaba ya wote, Kamanda wa ulinzi na usalama wa Italia katika mji wa  Vatican Maria Rosaria Maiorino,  alisema anayo furaha ya kumsalimia kwa niaba ya wote ikiwa ni ratiba yao ya kila mwaka kukutana naye,na kwa upande wake akisema ni shahuku kubwa kama kamanda wa kikosi cha ulinzi wa raia  katika mji wake.

Aidha alisema natoa salama na matashi mema ya mwaka mpya ambao umeanza hivi karibuni  kutoka kwa Kamanda Mkuu wa Polisi , na Mkurungenzi Mkuu wa Ulinzi na usalama wa raia Bwana Franco Gabrielli, ambaye hakuweza kufika kutokana na sababu zisizoweza kuzuilika,pamoja na hayo amewakilishwa na Kaimu wake Bwana Luigi Savina, Mkuu wa Polisi  Gianfelice Bellesini, Padre anayetoa huduma katika Kanisa lao, na mapaolisi wote wa Ulinzi wa Taifa kwa uapande wa Vatican waliokuwa wameshiriki katika mkutano huo."Na kwa namna ya pekee, ninapenda kutoa salama zangu za dhati kwa walinzi wa usalama wa papa kutoka Uswis na walinzi wa  usalama wa Vatican,ambao wamekuwa nasi bega kwa bega katika shughuli za ulinzi na usalama kwa dhati ni marafiki wa kweli". Alisema Kamanda Maiorino.

"Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu ulio malizika muda mfupi  ni mamilioni ya watu walifika kutoka pande zote za dunia, ili kuingia katika nyumba ya Mtakatifu Petro, kusikiliza maneno yako.Kwa upande wetu  wa ulinzi na usalama , ilikuwa mwaka wa shughuli kubwa ulikuwa umejaa matukio mengi, lakini tuliweza kufanya kazi kwa utulivuna kwa kutiii kanuni ya Mtakatifu Benedikto ambayo ina shirikisha mambo yote mawili ya kazi na sala.
Wito wako wa kila siku Baba Mtakatifu,juu ya  msingi wa maisha ya binadamu, kama vile msamaha, maridhiano, na upendo ni vitu ambavyo vimekuwa , msingi na nguzo  yetu ya kusimamia kidete  katika shughuli za kila siku na wenzangu tunao shirikiana pamoja katika kazi na pia  katika kutunza familia zetu.

"Tumeishi kipindi cha Jubilei ya huruma ya Mungu  kama fursa ya kukua kiimani na  imetuwezesha kufanya kazi bila kuchoka kutokana na na kusikiliza wito wako wewe Baba Mtakatifu wa kutuhimiza tuwe chombo cha maridhiano na kuwa wajenzi wa madaraja,pia  kupanda mbegu za amani".
Halikadhalika anasema, "kwa sasa tunaishi kipindi kigumu kisicho kuwa  na uhakika, kutokana na hali ya kutaka kwenda kinyume na maadili , yaani kwa mtazamo wa dunia. Lakini kwa wito wako wenye nguvu umetuhimiza na kutuamsha tuendelee na shughuli zetu kwa kuhakikisha   kwamba ulinzi na usalama wa raia unaedelea kuwepo daima , tukiutenda kiustadi na uwajibikaji,vilevile kuwa na subiria ya kila siku kwa ajili ya wote, watalii, waamini na mahujaji wote. Alimalizia akisema "tuinue mioyo yetu pamoja na kutamani  huruma ya Mungu ili atuzidishie kuwa na imani ya kweli katika kuhamasisha amani , ukweli upendo na uhuru.Na kwa maneno hayo ninajiweka mikononi mwako  tukiwa na matumaini ya kupata baraka kwa wote , kwaajili ya familia zetu na kwaajili kazi zetu.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.