2017-01-05 13:18:00

Wito wa kudumisha amani watolewa na Askofu mteule wa Jimbo la Chimoio


Askofu mteule João Carlos  Hatoa Nunes wa Jimbo Katoliki Chimoio ametoa wito wa ujenzi na udumishaji amani wakati akihojiana na  mwakilishi wa Radio Vatican mjini Maputo Hermínio José kwamba, ni kuhakikisha   amani katika nchi kama ilivyotangazwa na  vyama vyote viwili , chama cha Serikali FRELIMO na cha upinzani RENAMO. Askofu litoa wito kwa vyama vyote viwili vya kisiasa kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha  kwamba  amani inapewa kipaumbele cha kwanza kitaifa, kwani amani ni jina jipya la maendeleo endelevu ya watu!

 Askofu João Carlos alisema Frelimo na Renamo wanahitaji  kusikiliza kilio cha watu walio na kiu ya amani na  alisisitiza kuwa watendaji wote wa sera za kisiasa katika mchakato wa Amani,wanapaswa kuwajibika.Kuna haja ya kufanya kile kinachowezekana kwaajili ya kutafuta Amani ya kudumu.
Muda mfupi baada ya Krismasi, Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi alinukuliwa na Radio ya  Msumbiji akisema kuwa "kuna kila sababu  ya kuwa  na matumaini kwamba amani na ufanisi inaweza kufikiwa mwaka 2017".

Rais Nyusi alibaini kwamba Kiongozi wa upinzani wa RENAMO , Afonso Dhlakama alimpigia simu , na wote wawili walipata muda mrefu wa mazungumzo ya simu yaliyokuwa ni yenye manufaa.Kiongozi huyo wa Taifa la   Msumbiji alionyesha utashi wa wazi wa kuwa na mazungumzo ya kisiasa na Dhlakama.
Dhlakama alitangaza kuongeza muda wa kusitisha mapigano ya muda mfupi wa chama chake 4 Machi 2017. Katika mkutano na wanahabari, Jumatatu 2 Januari 2017 , Dhlakama alionyesha kuridhika  kutokana na uhakika kutoka  kwa Rais Nyusi kwamba vikosi vya usalama wa serikali watajiepusha na kushambulia RENAMO na kuacha utekaji nyara  wa  wanachama na wajumbe wake. Katika ujumbe wa Siku ya 50 ya Kuombea Amani Duniani kwa mwaka 2017 Baba Mtakatifu Francisko ametoa wito wa kurudia upya utamaduni wa kutokutumia nguvu, na kuujulisha ulimwengu na wadau wa siasa za kimataifa  kwamba majibu ya migogoro kwa njia ya vita ni kuzaa vurugu zaidi.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.