Mwananchi wa Misri na mkristo wa kikoptiki aliuwawa kinyama huko Alessandria
Misri tarehe 3 Januari 2017 na kijana mmoja akitoa sauti ya “Allahu Akbar”.
Hayo yalisemwa na Televisheni ya Al-Arabiya, na muuaji huyo alipatikana na kukamatwa
ndani ya masaa 24 kutokana na mitambo ya ulinzi ya kupiga picha iliyowekwa katika
maduka mbalimbali.
Kupatikana kwake ilitokana na picha zilizoonesha tendo la muuaji kumfikia mtu akiwa amekaa na kuchomoa kisu mfukoni na kumkata shingo na baaaye mtu huyo kutoroka.
Hili tukio limejitokeza wakati Jumuiya ya Kikoptiki ya huko Alessandria wanajiandaa
kusheherekea sikukuu ya kuzaliwa kwa Bwana ikiwa ni liturjia ya Kiotodosi, itakayofanyika
tarehe 7 Januari 2017, na tukio hilo limeaacha watu bumbuazi.
Wakati wakitafuta mwelekeo wa kisiasa wa huyo muuaji,wapelelezi wanafikiri labda
ni kwasababu ya kuuza vinywaji vya kulevya katika duka la huyo mtu aliye uwawa kinyama
.
All the contents on this site are copyrighted ©. |