Katika Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ambaye alianza kazi rasmi tarehe
1 januari 2017, alitaka dunia kuungana naye katika kusaka suluhu ya matatizo lukuki
yanayoikabili sayari hiyo.
Guterres ambaye alianza rasmi jukumu lake hilo, alisema hayo katika ujumbe wake
wa amani kwa jumuiya ya kimataifa akisema mwaka wa 2017 uwe wenye nuru na utatuzi
akisisitiza; "Katika siku hii ya mwaka mpya, nawasihi nyote muungane nami kuweka azimio
la pamoja la mwaka mpya: Hebu na tuazimie kuweka mbele amani. Hebu na tuufanye mwaka
2017, uwe mwaka ambao kwao sisi sote, raia, serikali, viongozi tunahangaika kumaliza
tofauti zetu.
Kuhusu madhila ya vita na athari zake Katibu Mkuu alisema hakuna mshindi zaidi ya
mateso kwa raia kwani ; "Makombora mazito yanaangukia raia. Wanawake, watoto na wanaume
wanauawa na wanajeruhiwa, wakilazimika kukimbia makwao, bila mali zao na kusalia hohehahe.
Hata hospitali na misafara inalengwa."
Hali kadhalika alizungumzia umuhimu wa mshikamano katika kufikia suluhu na kusema
"Kuanzia mshikamano na upendo kwenye maisha yetu ya kila siku hadi mazungumzo na
kuheshimiana katika migawanyiko yetu ya kisiasa….Kuanzia kusitisha mapigano kwenye
maeneo ya vita hadi kulegeza misimamo kwenye meza za mazungumzo na kufikia suluhu
ya kisiasa.Amani lazima iwe lengo na mwongozo wetu."
Na Idhaa ya Radio ya UM
All the contents on this site are copyrighted ©. |