2016-12-28 15:41:00

Padre Joseph Marie ateuliwa kuwa Askofu wa Jimbo la Mbalmayo


Baba Mtakatifu Francisko amepokea ombi la kustaafu  shughuli za kitume kwa  Jimbo la Mbalmayo huko Cameroon kutoka kwa Askofu Adalbert Ndzana na kumteua Mheshimiwa Padre Joseph Marie Ndi- Okalla kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki aliyekuwa Gombera wa Chuo Kikuu Katoliki cha Afrika ya Kati (Yaundè) na Katibu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Cameroon kwa ajili ya Mafundisho Jamii ya Kanisa. Askofu mteule Joseph Marie Ndi-Okalla alizaliwa 21 Novemba 1957 huko Douala. Baada ya masomo yake ya shule ya msingi aliingia seminari ndogo ya Mbalmayo. Aliendelea na masomo yake ya filosofía kwa mwaka mmoja katika seminari ya  Mama yetu Maria mkingiwa wa dhambi ya asili wa  Nkolbison, Yaoundé.


Aliendelea na masomo yake ya juu huko Ufaransa katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki mjini Paris na Chuo Kikuu cha Sorbona kwa masomo ya Taalimungu, historia na Mafundisho Jamii ya Kanisa. Alipata  shahada ya uzaminivu katika taalimungu. Jimbo la Mbalmayo liliundwa mwaka 1961 chini ya Jimbo kuu la Younde lenye wakazi 400,000 kati yao  250 ,000 ni wakatoliki.Jimbo hilo lina  parokia 87 , na linaloshugulikiwa na utume wa  mapadre 102 kati yao 77 ni mapadre wa jimbo na 25 mapadre wa mashirika ya kitawa, wapo watawa  wakike 40 na waseminari 66.

Sr Angela Rwezaula.

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.