2016-12-27 17:12:00

Yerusalemu inaweza kujengwa tu kwa kuheshimu utakatifu wa watoto


Patriaki Bartolomeo I wa Kanisa la Kiorthodox la Costantinopili, ameamua kuutangaza mwaka 2017 kuwa ni mwaka wa "Utakatifu wa Mtoto"; Aliyathibitisha hayo mwenyewe wakati wa mahubiri yake ya sikukuu ya Noeli kwa Mwaka 2016. Wito wa Patriaki wa Kiotodosi umemsukuma kutafakari maajabu ya kuzaliwa kwa Yesu kwa kutumia “ Ni neno la Mungu akafanyika mwili na akaja kwetu” na kusema ni  yeye aliyekuja kwetu kama  mtoto Yesu, ni Mkuu wa Ulimwengu uliokuwa unataka kumuondoa. Katika Injili ya Mathayo inasema,mnapaswa kuwatunza watoto na kuwalinda , maana ni waathirika , ni lazima kuheshimu utakatifu wa watoto hao, alisema.

Patriaki Bartolomeo anasema watoto siyo kwamba ni waathirika tu  wa vita na uhamiaji wa kushurutisha, bali ni waathirika hata katika nchi zenye maendeleo kiuchumi na  kisiasa ulimwenguni, na kufafanua ya kuwa ni kwa upande wa kipeo cha ndoa ,talaka za ndoa ndani ya familia, ambazo uwapelekea  watoto  kuathirika na aina mbalimbali za mateso ya kimwili na kiroho. Patriaki Bartolomeo vilevile alionyesha  pia njia nyingine  zinazoathiri watoto  wa leo  hii akisema  ni njia ya mitandoa ya kijamii kama vile televisheni na intaneti, huo ni uchumi wa ufujaji unao wageuza watoto wakiwa bado wadogo kunaswa tayari kwenye matendo ya ufujaji na  anasa. 

Aidha katika ujumbe wake Patriaki alitumia maneno ya Yesu anavyoelezea watoto akisema , Kanisa letu Taktifu linatuaalika “ tuwe kama watoto, kwani kama hatugeuki kuwa watoto wadogo , hatutaweza kuingia katika ufalme wa mbingu,vilevile hasiye pokea ufalme wa mbingu kama watoto wadogo hataingia katika ufalme huo. Katika fumbo la Kuzaliwa kwa Bwana kwa upande wa Patriaki amefupisha  kwa  maneno ya  kiitikio cha sikukuu ya kuzaliwa kwa Bwana kinachosema “mtoto amezaliwa kwaajili yetu, ni Mungu wa nyakati zote”  na kusema “Mungu anajionesha katika  ulimwengu akiwa na moyo safi na mwepesi  kama mtoto mdogo” na kuongeza ni  kwa sababu watoto  wanatambua mapema ukweli, unaofichika  kwa  watu wenye hekima. Alimalizia  kwa maneno kutoka kwa mtunzi wa  mashairi ya kigiriki  maneno yasemayo “Ni kwa njia ya watoto tu unaweza kuujenga mji wa Yerusalemu”.

Sr Angela Rwezaula.

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.








All the contents on this site are copyrighted ©.