2016-12-21 15:12:00

Kardinali Bagnasco asema, tusikilize ndani ya moyo maswali ya kweli


Kardinali Angelo Bagnasco Rais wa Baraza la Maaskofu nchini Italia aliadhimisha Ibada ya misa kabla ya sikukuu ya kuzaliwa kwa Bwana kwa wana Bunge la Serikali ya nchi Italia Jumanne 20 Desemba, 2016  kwenye  Basilika ya Mt. Maria sopra  Minerva Roma.


Akianza mahubiri Kardinali alisema , inarudi tena  utamaduni wa Misa kabla ya Kuzaliwa kwa Bwana, akiwasalimia viongozi kuanzia ngazi ya juu, bila kumsahau Monsinyo  Lorenzo Leuzzi Askofu msaidizi wa jimbo la Roma anayetoa huduma katika Kanisa lililoko katika Bunge la Italia na kusema , anatafsiri utume wa Kristo,  wa kuwapo pale watu wanapofanyia kazi. Ni ukaribu ambao hasa Injili ina onesha njia ya kweli  na  makusudi ya siasa.

Tunatambua ya kwamba imani si mawazo wala sheria, bali ni kitendo cha mtu binafsi  kukutana  na Kristo: Alieleza, maana yeye ni mwana wa Mungu milele, mkombozi wa dunia , ni kitovu cha historia  ni mwanzo wa uumbaji , na mwisho wake. Yeye ni mkate wa uzima usio isha , ni jua la matumaini, ni siku isiyo na machweo, ni joto linalopasha mioyo. Na kwahiyo  bila yeye maswali makubwa hayawezi kujibiwa, na binadamu ubaki na  fumbo lake mwenyewe, bila yeye tegemeo la roho na ya furaha ya maisha ,hakika maisha  uangukia katika utupu.


Kardinali Bangnasco akitazama hali ya sasa ya mashambulizi ya ovyo kila kona , aliendelea kusema  uzoefu wa sasa tena unaonyesha matukio  ya damu ambayo yameikumba nchi ya Ujerman na Uturuki, na kuongezea chuki na hasira kwa watu, hivyo tukiwa katika kusali kwaajili  ya waliopoteza maisha yao na kujeruhiwa  dhidi ya machafuko hayo , tumuombe Mfalme wa amani alete juhudi za haki na maridhiano.


Uzoefu wetu tulio nao unatuakikishia ya kwamba hata furaha  na mafanikio binafsi haviwezi kamwe kuujaza moyo, Aliuliza swali ,Je ni kitu gani kinakosekana katika usalama wa binadamu ili kuwa na  hali nzuri , afya, umri , nafasi na upendo? 
Kwanini tunaishi  kwa kujisikia upungufu wa  vitu hivyo rohoni mwetu  na kujisikia msukumo wa kwenda  mbele zaidi?

Aliendelea ya kwamba jibu hili liko katika uzoefu :vipindi vizuri daima havikamiliki bali viko katika mwendo, kwa maneno zaidi ni dhaifu, wakati sisi daima tunataka kujisikia tumejazwa kabisa. Shahuku hiyo  inajitokeza katka  aina nyingi lakini daima ma mahali popote  mikujisikia ukosefu ukosefu wa kitu flani.Haiwezekani kamwe kuishi kwa  siku peke yako , ukiwa unafikiria mambo yako madogo  binafsi, na hata kama ni makubwa hayawezi kuujaza moyo wako : Je kama hayo yote uliyofanya, baadaye yatakwisha , nini maana ya kijitoa sadaka katika maisha?.

 

Leo hii tunaishi kama vile watu ambao tumejisahau, na daima tumeweka viini  machoni ya  kushinda katika kazi, uwajibikaji muhimu. Na hii ni kuvutiwa na utamaduni unaotutaka tuishi kiusahaulifu. Nia kubwa hasa ni ile ya kutukataza tusifikiri, tusisikilize sauti ndani ya mioyo yetu,  ya kujiuliza maswali ya msingi kama vile nini maana ya kuishi,maana ya kifo na mengine zaidi, je ni muhimu kuishi.

Kardinali aliendelea,  usikila maswali hayo ndani ya mioyo yetu  maana yake ni kuelekea katika uwanja  wa ukweli , mambo yalivyo kweli na siyo jinsi wanavyotaka tuamini , na jinsi gani tunavyojidanyanya sisi; maana yake nafsi ytu inapata uhamsho  katika uhuru, na mwisho  wake  ni kuona kitu gani chenye manufaa na cha  kuangaza .


Aidha Kardinli alichambua maana yake zaidi alisema  ni kelele na picha ambazo hujaribu kuchuka nafasi na kuzuia ukimya uweze kuingia ndani mwetu, wa kufikiria ukweli, alionya ;  hakika ni hatari kufanya mawazo yanayojenga manufaa binafsi.
Lakini basi je kuna maana gani ya  maisha na hasa kwa mtazamo wa kijujuu wa kujaza nafsi? Licha ya mafaniko ya kisayansi na kiteknolija binadamu kamili ni yule anayetambua  mafanikio hayatokani na mikono yake mwenyewe na wala ukamilifu daima kuwa  ni wa kazi yake mwenyewe , bali unatoka sehemu nyingine zaidi,na unakuja kutoka juu kama zawadi.

 
 Kutoka juu imejionesha kwa Jina la Yesu , Mungu anayeokoa  ni  Emmanuel, yaani Mungu pamoja nasi.Yeye alikuja tangu kale kwasababu ya kutufungulia umilele,na kutuzawadia umilele huo kwa hali ya  unyenyekevu ili nasi tupate kuwa wakubwa,hata  katika umasikini , kutuvisha ili nasi tuwe matajiri wa watoto wa Mungu . 

Yeye alitutafungulia kitabu cha maisha , njia ya binadamu wa kweli , katika furaha kamilifu. Binadamu  anashiriki katika kazi, lakini si mhusika mkuu, bali hiyo humsaidia yeye  kuishi.
Mwisho alimalizia Kardinali Bagnasco  akisema, katika sherehe za kuzaliwa kwa Bwana, tunataka kumuomba mtoto Yesu ili tuwe wenye hekima na huru, kwaajili ya roho zetu na kwaajili maana wa nyakati zetu katika kujenga manufaa ya wote.

 

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.








All the contents on this site are copyrighted ©.