2016-12-19 15:44:00

Vatican yasema Usafirishaji wa binadamu ni mojawapo ya uhalifu wa kutisha


Vatican inataka wanachama wa Shirika la Usalama na Ushirikiano wa nchi Barani Ulaya kutambua biashara ya binadamu kama moja ya uhalifu wa kutisha na kufanya kila liwezekanalo kutokomeza mizizi  yake. Ni maneno ya hotuba ya Munsinyo  Janusz Urganczyk, mwakililishi wa Vatican  katika Baraza la kudumu katika masuala ya usalama na ushirikiano wa Ulaya (Osce), Alhamisi 15 Desemba 2016 wakati wa mkutano  wao wa 1124 wa Mwaka  huko Vienna.


Alisema ,Vatican mara nyingi imesema juu ya shetani  dhidi ya maovu ya biashara ya binadamu, kazi ya kulazimishwa na aina zote za utumwa mamboleo, mara nyingi ulenga unyonyaji  na kuwawazia  watoto. Hii imesemwa bila kuchoka kwaajili ya kuchukuliwa  hatua, kupitia taasisi za Kanisa Katoliki  dunia ni kote ili kukomesha mara moja hali  ambayo ni “kansa ya kijamii”ambayo ni mojawapo ya changamoto kubwa za nyakati zetu kama mapapa walivyosisistiza mara nyingi.


Idha aliendelea , Kwa maongozi ya mafundisho ya kanisa, hasa  tangu Mtaguso wa  Pili wa Vatican uanze , kama ilivyoandaliwa na mapapa John Paul II, Benedict XVI na Francis, taasisi nyingi  kikatoliki , maparokia, mashirika ya hisani na makundi ya walei kutoka sehemu mbalimbali za dunia zimekuwa na nia kila  siku ya mapambano dhidi ya biashara haramu, kwa njia ya kinga na kuwatunza waathirika. Akieleza njia hizo Monsinyo alisema ;
Katika kupinga mtandao halifu, waliamua kujenga  imara mshikamano wa mtandao,  wapate kukutana mara kwa mara katika kuwasiliana, na pia kupitia katika vyombo vya habari  za kijamii, ambayo inaruhusu  kubadilishana  habari na mipango kwa haraka . Wao pia wanashirikiana na Serikali, serikali za mitaa ili kuwatia moyo katika maamuzi yao ya kisiasa.


Alitoa mfano ya kwamba : Kama watangulizi wa Papa Francis walilaani tatizo hili kubwa sana na linaloficha  siriili lichukuliwe hatua madhubuti .2014 akiongoza Azimio la Pamoja na Viongozi wa dini dhidi ya utumwa  wa kisasa wa  mamboleo  aliamua  kuundwa chombo kinachojulikana "kikundi cha Mt.  Marta Group", Jina hilo baada ya kuwa ndiyo makazi yake huko Vatican.
Hii ni muungano wa wajibu kati ya vikosi vya polisi na viongozi wa Kanisa duniani kote, ambao una lengo, pamoja na vyama vya kijamii, ili kutokomeza biashara haramu ya binadamu na kuendeleza mikakati ya kuzuia na kuwaunganisha na jamii ya waathirika, pamoja na kuhakikisha huduma zao za kichungaji.


Shukrani ziwandee makundi ya kazi ,ikiwa ni pamoja na ushirikiano wa karibu kati ya Kanisa na Polisi,wengi wanao angaika na kukaa kimya lakini wanasikia.Hawa ndiyo Papa Francis alisema,” kinachohitajika nguvu ya pamoja, ufanisi , ari na juhudi, kwa pamoja ili kuondokana na sababau ya jambo hili lenye utata,pia ni kukutana  na kusaidia  watu ambao uanguka katika mtego wa biashara “ni  ambao kwa walio wengi  hawawezi kujitetea, ni kuwaibia utu wao ,uadilifu wao kimwili na kisaikolojia, na hata maisha yao.


Katika mkataba wa agenda ya 2030 ya Dunia wa hivi karibuni na (SDGs) hasa wa lengo la 8.9 ya wanachama wa Umoja wa Mataifa ulisaini maadili yao muhimu ya kupambana na ukiukaji huu mkubwa wa haki za msingi za binadamu, sambamba na hiyo  Vatican inawataka Mataifa yote yanaoshiriki, kutambua kwamba  usafirishaji wa binadamu kama ni mojawapo ya uhalifu wa kutisha unaondelea  kuharibu wajibu wao kimaadili, na hivyo ni muhimu kushughulikia ipasavyo na kutokomeza ki ukweli.


Umakini lazima utolewe na hasa kwa kutokomeza uhalifu huu na hasa unapowashambulia watoto, ambao ni watumwa , na uangukia mawindoni na kunyonywa kama vibarua au askari, na baadaye uangukia katika mtandao wa kusafirisha madawa ya kulevya au kuingizwa kwenye picha chafu ;ni wale  wanao lazimika  kukimbia kutokana na migogoro, uhatarisha kutengwa au kutelekezwa.

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.