2016-12-12 16:34:00

Ewe Mwenyezi Mungu wewe umenidanganya , nami kweli nimedanganyika


Jumapili 11 Desemba Kardinali Pietro Parolini Katibu wa Vatikan, alitoa daraja la mapadre 36 wa Shirila la Legionari wa Kristo (Legionari di Cristo) Kwenye Basilika ya Ya mtakatidu Yohane wa Laterano.
Mapadre wapya 36 ni wa kutoka katika nchi mbalimbali na hivyo Kardinali Parolini katika Omelia yake alisema,  safari yao kutoka pande zote za dunia, Argentina , Brazir, Cile, Ufaransa, Ujermani, Uingereza, Italia, Mexico, Marekani na  Venezuela inayo sababu moja ya msingi itokayo katika kitabu cha Yeremia , Ewe Mwenyezi Mungu wewe umenidanganya , nami  kweli  nimedanganyika , wewe una nguvu  kuliko mimi nawe   umeshinda.(20,7) na hiyo  ni sababu ya kuacha mvuto wa Yesu Kristo kama asemavyo Mtume Paulo kwa wafilipi(Fil,3,12) mpatie Mungu nafasi ya kwanza katika maisha yako.


Ni furaha kubwa kwa wito wao huo na aliwashukuru  wote walio wasaidia kufika hatua hiyo,kuanzia  familia zao, Jumuiya za parokia wanakotoka ,  walimu wao wa Shirika la Legionari wa.
Pia aliwashukuru pia walioudhuria ibada hiyo, na kuifanya iwe yenye kupendeza kwa furaha  na  kuendelea , wamejitoa kwa  Bwana ili wawe wamisionari wa Injili kati ya watu.Ni kwa njia ya Roho Mkatifu katika mikono ya  upako itawawezesha kutoa huduma  kama mitume  wa Bwana kati ya watu, na kwasababu hiyo kila muumini anaweza kukutana na  Kristo kwa njia ya kueneza Neno la Bwana  linalookoa,  katika maadhimisho ya ibada na sakramenti mbalimbali ambazo ndizo ishala muhimu za uwepo wake. Ishala hizo ugeuza  maisha na kuyatakatifuza, ni kwaajili ya huduma hiyo ya kitume ambayo ndani ya mioyo yenu iwaongoze kila siku.


 Katika somo la kwanza tumesikia maneno ya Nabii Isaya yanayochangamsha  nafsi ya utume wake ,  kwa maneno hayo yanapata fursa kwa upande wenu sasa “Roho wa Mungu yupo pamoja nami , na Bwana amenipaka Mafuta (Is 61,1 )
Kiongozi wa kwanza katika tukio hili ni roho wa Bwana , kwa njia ya upako wa mafuta muweze kuwa chumbo hai  pekee cha uchunganji  na mpate  kwa namna ya pekee kuwa mwakuhani wa Kristo mkitenda katika jina lake. Ni Mungu anayewateua na kuwapaka mafuta, ni Mungu anayewatuma kwenda kupeleka habari njema kwa wenye shida , kuwafariji walio pondeka mioyo, na kuwatangazia mwaka wa neema wa Bwana , muwe ishala inayoonyesha   upendo wake mwanifu na huruma , ambayo haichoki kamwe  kutafuta kila mtoto aliyepotea, amechoka na kuta tamaa mbele ya changamoto za sasa.


Akitoa wito juu ya utume wao ,Mapadre wapya aliwa’galisha kujiweka tayari kukabiliana na ulimwengu huu akisema   maisha yao daima ya kitume hayatakuwa ni rahisi maana kuna hali ya kuchukiwa na pia  mitafaruko ya dunia hii, bali kutokana na watu kuwa na uhusiano wa Mungu, watakutana pia na watu wenye ut una wanao mcha Mungu.Hali ya kuchukiwa hata Yesu mwenyewe aliitambua na ndiyo maana tunasoma katika Injili ya Yohanne  17,9.15 Yesu akisali kwaajili ya mitume katika ulimwingu hu il Mungu aweze kuwalinda na mabaya yote kwa maana wao wanaishi katika ulimwengu bali siyo wa ulimwengu huu.
Alimalizia akiwaombea  Roho Mtakatifu anayekuja washukie zaidi juu yamo  awaimarishe na familia yao  ya Legionari wa Kristo  ili kila mmoja wao awe mwaminifu katika wito wake wa kikuhani.

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.