2016-12-08 15:35:00

“Wahamiaji ni ndugu zetu”kaulimbiu ya Mkutano wa Mamea 80 wa miji Vatican


Pamoja na Kauli mbiu ya  Mkutano huo wa Ijumaa 9-10 Desemba wa Mamea 80 wa miji kutoka duniani kote  , watajadili mambo mengi zaidi  ambayo yatawakilishwa na mawazo ya maoni ya umma ya Kimataifa na hasa katika mtazamo wa  ongezeka la idadi ya wakimbizi katika sayari yetu, kutokana na vita , njaa na majanga ya asili. Ratiba inasema washiriki wa Mkutano huo wanatazamiwa Jumamosi 10 Desemba  mchana  kukutana na baba mtakatifu Francisko.


Masuala ya vizuizi vya kujenga kuta za ziada na ngome, hautazuia  mamilioni ya wahamiaji wanaokimbilia kutokana na vurugu , umasikini uliokithiri ,maradhi, ukame au mafuriko,  bali ni ushirikiano wa kimataifa kwa ajili ya mafaniko ya haki za kijamii unaoweza kuleta ufumbuzi wa dharura hizi.Aidha maelezo kuhusu mkutano huo wa mamea  katika Chuo cha Kipapa cha Kisayansi wanayo lengo la kuanzisha taadhari ya kimataifa  juu ya tishio linaloikumba Dunia  na kuweza kutafuta mwafaka kwa  utulivu  hasa  kutokana na kuongezeka hilo la wakimbizi katika Sayari yetu, ambayo inakadiriwa kuwa ni zaidi ya milioni 125. 


Kati ya sababu kubwa ya watu tatu robo ya dunia kuwa na haja ya msaada wa kibinadamu ,na kulazimika kuondoka katika nchi zao ni vita, na inayobaki  ya dharura ya kibinadamu  inayowarudisha nyuma ni kutokakana na majanga ya asili ambayo kwa miaka ya hivi karibuni imezidi kuongezeka na kuleta migogoro ya mazingira kama vile njaa, mafuriko  na dhuroba kali kutokana na mabadiliko ya Tabia nchi na hasa kwasababu ya ku ukataji wa miti hovyo, na matumizi  mabovu ya kilimo kwa ujumla amabayo uchangia kiasi kikubwa cha majanga ya maszingira.
Katika mada  karibia 6 watakazo gusia  kwenye mkutano wa Vatican wataangalia  njia mpya ya kutafuta milango ya usalama inayojulikana kimataifa na katika umoja wa nchi za Ulaya kwa lengo la kuwafanya watu wawe wamoja na kujali heshima za kibinadamu kwa wakimbzi wote. Na  namna ya kutafuta mbinu za kuondokana na mabadiliko ya tabia nchi.


Kwa namna hiyo  Mkutano wa Mamea hao 80 kutoka dunia nzima katika nyumba ya Casina Pio IV, utakuwa wa kutathmini mapendekezo angalau sita katika suala hili: kumaliza vita nchini Syria, na kuzuia wimbi la wakimbizi, kuhusu Brexit ya Uingereza, kufikiria juu ya ubunifu zaidi wa kuzaa matunda ili kuleta muungano badala ya mafarakano kwa kuzingatia  kipaumbele cha wahamiaji na ukosefu wa kazi .
Kuunda   njia za kibinadamu zenye usalama na za kuaminika, kuheshimu kanuni msingi na ufuatiliaji, kutafuta ufumbuzi wa makundi ya waathirika wa biashara ya binadamu, kurejesha  hisia ya  haki na fursa za haki, vijana hawana ajira na mazingira magumu, katika makundi ya kijamii  maendeleo ya kiuchumi katika nchi zenye kipato cha chini. Haya yote ni pamoja na mwongozo wa waraka wa Baba Mtakatifu Francisko wa “Laudato Si”.

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.