2016-12-07 14:55:00

Ujumbe wa Baraza la Maaskofu wa Burundi wa kufunga Mwaka wa Jubilei ya Huruma


Ujumbe kutoka  Baraza la maaskofu wa Burundi wakitoa pongezi kwa hatua ndogondogo zilizofanywa na wanachi  katika maridhiano , na kuwashukuru wote walioshiriki kukuza njia ya maridhiano  katika ujumbe wa kufunga mwaka wa Jubilei ya huruma uliyotolewa na Shirika la Habari la Fides.

Katika ujumbe wa  kufungua  mwaka wa huruma 2015, Maaskofu wa Burundi waliwaalika na kuwa  na mategemeo ya wana Burundi kutumia mwafaka wa Jubilei ya huruma katika  kufanya maridhiano , na  kuweza kukaa kwa pamoja ,na kuamua ukweli katika majadiliano ya wazi,ili wapate   kutatua matatizo ya nchi na ya kwamba nchi ya Burundi iweze kuishi kwa Amani,na kwa ulinzi.

Lakini katika ujumbe huo Maaskofu wanabaini ya kwamba bado kuna ndugu kaka na dada waliokimbilia  nchi nyigine  , pamoja na kusikia wito wao, hawakukubali kurudi makwao kwasasababu bado hajisikiii kuwa na ulinzi na usalama wa nchi. Wanauliza swali katika ujumbe huo, je hakuna cha kusahihisha kwasababu ya kutokujisikia usalama na  kulindwa?

Aidha Maaskofu wanatoa malalamiko juu ya  watu walio baki katika mazingira nchi ya kwamba hawaaminiani ,kwasababu inaoneka wanashitakiana wao kwa wao, wakiwa na uoga wa kusema ukweli kwa sauti kubwa, na pia  wanaishi bila  kuaminiana katika nyumba za jirani na kumbe ni mwafaka wa kuweza kusema ukweli na kuupokea ukweli ambao uokoa na kuleta maridhiano.

Migogoro ya   siasa huko Burundi imeanza tangu  mwezi wa 4, 2015 , wakati Rais Pierre Nkurunziza alipoamua kugombea kwa mara ya tatu urais, kwa kukiuka sheria ya katiba na makubaliano ya amani huko Arusha nchini Tanzania.

Tukio hilo la Nkurunzinza kwa mwezi wa 7 ilisababisha hali mbaya na fujo, ghasia  , mauaji , na kupotea kwabaadhi ya wapinzani wa vyama vya kisisasa , na kuundwa kwa makundi ya kigahidi  wa kupinga Nkurunziza; na machafuko hayo hadi sasa  yamesasabisha mauji ya watu 500 na 300,000 kukimbilia nchi zinazopakana na Burundi.

Sr A.Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.