2016-12-05 15:09:00

Biashara kufikia malengo ya agenda ya 2030 kwa maendeleo endelevu .


Akihutumbia  katika Baraza la kudumu la Ushirikiano wa kibiashara wa nchi za nje na za Kimataifa   Monsinyo Ivan Jurkovic mwakilishi wa Vatican katika Baraza hilo alisema ni muhimu  kutafsiri  juu ya biashara ili kufikia  makubaliano na malengo ya agenda ya 2030 kwa maendeleo endelevu .


Pamoja na wasiwasi uliopo juu  faida za  biashara huria   ya dunia na juhudi  zake zilizopigwa kwa siku za karibuni , bado juhudi zinapaswa kufanywa na Jumuiya ya Kimataifa ili kuwawezesha wanabiashara huria wa nchi zinazopiga maendeleo ili kuingia katika muungnano wa biashara wa kidunia.
Monsinyo Ivan alisema  Uchumi wa kidunia unajitahidi kutaka kuondokana na kipeo chake  ambapo kwa mwaka 2008 -2009 ulitia uzito kwa mataifa yaliyo masikini na hata katika uchumi wa viwanda ulio na utofauti. Mbele ya matukio kama hayo  changamoto kubwa ya kisiasa waliyo nayo kwenye Jumuiya za Kimataifa , ni ule uzito wa utandawazi ambao lazima kuunda na kujenga utajiri unaogawanywa kwa pamoja.


Ili kufanya hivyo aliendelea Monsinyo, Taasisi za kisiasa na malengo 17 ya Agenda  ya maendeleo  yaliyokusundiwa tangu 2015  hawawezi kuzuia kudumisha uwiano katika maslahi maalum , bali lazima manufaa yawe kwa wote. Lakini hiyo inahita uangalizi wa pande zote kwa kila mwanachama wa Jumuiya ya Kimataifa na ushirikiano kutoka katika upande wa nchi masikini.


Alimalizia  akisema Monsinyo Ivan ya kwamba kama  kweli wanataka   kufanikiwa katika Agenda 2030 wanapaswa  kuendeleza mipango ya maendeleo  iliyokubaliwa huko (Addis Ababa Action) Agenda mwaka 2015 kwenye mkutano wa tatu wa Umoja wa Mataifa juu ya mikopo ya fedha kwaajili ya  maendeleo , na lengo kubwa  ni mabadiliko  na hasa mipango iliyokusudiwa iwekwe kwenye matendo.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.