2016-12-01 15:58:00

Madaktari na Afrika Cuamm wanafanya juhudi ya kupambana na janga la ukimwi


Desemba mosi  ya kila mwaka ni siku ya ukimwi duniani. Madaktari na  Afrika Cuamm wanafanya juhudi ya kupambana na janga la ukimwi  kwa mipango mbalimbali barani Afrika. Katika nchi ya Tanzania na  Msumbiji  mpango wa kuzuia na kukinga ugonjwa wa ukimwi  unaoendelea  kwa kasi.Novemba 30 -1 Desemba  2016 mji wa Padua umefanyika kongamano kwa ajili ya  kuhamasisha nguvu la kupambana na virusi hivyo  Afrika mahali ambapo tatizo la ugonjwa wa ukimwi unaendelea. Na katika mji wa Beira nchini  Msumbiji , walifanya maandamano makubwa   wakiwa na madaktari na  Afrika Cuamm. Vituo vidogo vidogo  vya afya vilivyo  tawanyika katika Bara la Afrika  kama vile kituo cha Bugisi Tanzania walifanya maandamano hayo ya kuhamasisha  mpango huo wa kupambana na ugonjwa wa ukimwi barani Afrika kukuba haja kubwa ya kuhamasisha

 Mwaka 2015, watu  15,700 wameweza kupatiwa matibabu na hawa madaktari na Afrika  na  daima wamekuwa mstari wa mbele katika harakati za kuzuia ukimwi. Ikumbukwe 1985 katika mkutano wa kwanza wa Madaktari wa CUAMM  wa Tanzania huko Tosamaganga , kikundi cha madaktari kutoka italia wa cuamm kwa mara ya kwanza waliongelea juu ya Ukimwi  wakijadili  utafiti wa wanasayansi  uliokuwa umefanyika katika hospitali ya Bukoba nchini Tanzania .Na baada ya mika 30  bado watu hawajatambua  tatito  linalo wakabili  au namna ya kuweza kujizuia wasiambukizwe na ugonjwa huo. Ndiyo lengo kuu la madaktari wa Afrika  cuamm kuweka mikakati ya  kuwasaidia ili watu wawe na haki ya kutibiwa.

Akiongea mkurugenzi wa madaktari  na Afrika Cuamm wakati wa tukio hilo Padre Dante Carraro alisema nchi 7 za kusini mwa  Jangwa la Sahara wanazofanya kazi  wanapambana na ugonjwa huo wa ukimwi na kuweka juhudi zaidi  kwenye mipango  ya kuwasaidia walioathirika na virusi hivyo.Padre Dante aliongeza ;  wanakazia hasa namna ya kujikinga kuondokana na kuambukizwa kutoka kwa mama na  mtoto , na kuwafundisha vijana  namna ya kujikinga  kwa kutumia vipimo (test and Treat). Nchini Tanzania katika mkoa wa Shinyanga wilaya ya Simiyu  mwezi Novemba  2016 walianzisha mpango wa miaka mitano ya kuwauguza watu 20,000 wenye  maambukizo ya  ukimwi kwa kutumia mbinu  ya (Test and Treat).

 Nchini ya Msumbiji madaktari na Afrika wanaendelea na  mbinu hizo za matibabu kwa asililima 15% ya watu wa Msubiji walio na virusi hivyo vya ukimwi, na zaidi ya hayo asilimia kubwa ni kwa ya vijana walioathirika na  virusi hivyo. Uganda kaskazini  kwenye  mkoa wa Karamoja ; Cuamm inasimamia mpango wa Serikali  wa kuzuia na kukinga virusi vya ukimwi kwa mama anapokuwa ni mjamzito .Madaktari na Afrika wanaendeleza Zaidi ya mipango maalumu  ya kupambana na virusi vya Ukimwi ,katika juhudi hizo kwenye mahospitali yote wanapofanyia kazi kuhakikisha wanaendeleza tiba ya wagonjwa wanapofika katika vituo hivyo .

Sr. Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.