2016-10-12 15:47:00

Papa akumbusha "tutahukumiwa kwa jinsi tunavyo wahurumia wengine "


Baba Mtakatifu Francisko katika Katekesi yake kwa mahujaji na wageni, ametoa mwaliko kwa watu wote kila siku kukumbuka akilini, fadhila na utendaji wa watu watakatifu kwa mfano Mama Tereza wa Calcutta, ambaye anaonyesha  waziwazi uso wa huruma wa Kristo , ulivyo na uwezo wa  kuleta mabadiliko makubwa katika utamaduni mahalia. Mafundisho ya Papa yalilenga Injili ya  Mtakatifu Mathayo, ambamo Bwana anatuambia kwamba tutahukumiwa kwa jinsi tunavyo wahurumia wengine.

Alisema kwa Jumatano hii, tukiendelea kuelekea katika kukamilika kwa  Jubilee maalum ya mwaka Mtakatifu wa huruma , ambamo katika katekesi zake amekuwa akiizungumzia   huruma ya Mungu inayoonekana  kupitia hasa  Mwana wa Mungu,  na  wajibu wetu, kama wafuasi wa Yesu, katika kuwa na  huruma,  kama Baba wa Mbinguni, pia anaendelea kuizungumzia huruma ya Mungu, kama ilivyoandikwa katika  Injili ya Mathayo, ambamo  Bwana anasema  kwamba,  tutahukumiwa kulingana na huruma tunayo mwonyesha kupitia kwa watu wanaotuzunguka ,wake kwa waume.

Papa Francisko ameeleza na kufanya rejea kwa maneno ya Yesu, alipowaambia wanafunzi wake ,” kuweni na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma” (Lk 6,36). Papa anasema , maneno haya  maana yake hasa yanailenga  katika  dhamiri na uhusiano wa kila Mkristo kwa watu wengine. Na kwamba katika ukweli wake,kuiishi huruma ya Mungu maana yake ni  kuwahurumia wengine. Na wale wanaopokea huruma hii , basi wanapaswa kuwa ishara na chombo kinachoibeba  huruma hiyo kwa ajili ya kuwafikishia watu wengine.  Huruma hii zaidi ya yote ,si tu kwa wakati fulani fulani lakini inapaswa kumwilishwa katika maisha  na utendaji wa  kila siku.

Papa alieleza na kuhoji kumbe basi ni kwa namna gani tunaweza kuwa mashahidi wa huruma ya Mungu?  Alijibu akisema ni vyepesi sana, kwa kuwa Bwana  huionyesha njia yenyewe kwamba,  si kwa matendo makubwa, lakini ni kupitia huduma ndogondogo tu katika maisha ya kawaida. Utendaji huo mdogomdogo mbele ya macho ya Bwana, huwa na thamani kubwa,  kama alivyokwisha sema Yesu kwamba,  tutahukumu kwa hayo. .  Yesu alisema, kila tunapotoa msaada kwa watu maskini na wanyonge wasiokuwa na kitu , kama kuwapa chakula, kinywaji, mavazi au kuwatembelea wagonjwa,wafungwa na walio katika dhiki, wafiwa  na  kukaribisha wageni , huko   ni kumhudia Yesu mwenyewe( Mt 25 -31-46).

Papa Francisko pamoja na kuzungumzia  matendo haya  aliyoyataja kwamba Kanisa huyaita  matendo ya huruma ya kimwili, kwa kuwa ni kumsaidia mtu mhitaji  kihali, pia alitaja kwamba, kuna matendo  mengine saba ya huruma ambayo ni  kiroho,  ambayo pia ni muhimu sana hasa katika nyakati hizi za leo , kwa kuwa hugusa moyo  wa mtu mwenyewe na kwa mara nyingi hutufanya kuteseka zaidi. Matendo hayo ni utoaji wa ushauri kwa wenye  mashaka, kuwafundisha wasiojua, kushauriana wenye dhambi,  kuwafaraji wanaoteseka, kusamehe mwenye  makosa, kuwa na uvumilivu wale wanaotukosea  na kuwaombea  walio hai na wafu.

Papa aliendelea kusema kwamba,  kwa ajili ya  kuonyesha imani hai, hayo yote na yafanyike kimyakimya bila mbwembwe,ila  kama utendaji wa  kawaida.  Alieleza na kutoa  mwaliko kwa watu wote kuyaishi hayo kwa kutazama mfano wa maisha ya Watakatifu kama vile Mama Teresa wa Calcutta, alivyo ionyesha na kuitangaza  sura yenye  huruma ya Kristo, inayoweza  kubadili utamaduni  wa wale walio karibu nasi. .  Papa aliomba daima na tuweke akilini mwetu haya huku tukijitahidi kuyaishi katika utendaji wa kila siku kimya kimya.

 Baada ya Katiekesi kama kawaida Papa alisalimu makundi mabalimbali yaliyofika kwa wingi kusikiliza kateksi yake , ambamo Jumatano  kwa wale waozungumza Kiingereza,  Afrika wengi walitoka Ghana, Namibia na  Nigeria. Kwao wote aliwatakia Jubilee njema  ya Mwaka wa Huruma , iweze kuwapa  neema ya kufanya mabadiliko ya kweli kiroho,  kwao wenyewe na kwa familia zao, pia akimtakia  kila mmoja wao furaha na amani katika Bwana wetu Yesu Kristo.








All the contents on this site are copyrighted ©.