2016-09-14 15:31:00

Papa: ataja njia nzuri ya kupambana na uchovu na kukatishwa tamaa.


Baba Mtakatifu Francisko katika Katekesi yake kwa majuaji na wageni, aliendelea kutafakari mwaka wa Huruma akiainisha matendo ya huruma ya Yesu, yaliyotajwa katika Injili  na sauti ya Yesu,  inayowaita waliokata tamaa,  maskini na watoto wadogo na dhaifu wote wasio kuwa na nguvu za kujiinua wenyewe, kutegemea nguvu za kipekee za Mungu” kama ilivyoandikwa katika  Injili  ya Matayo 11: 28-30 ” Njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo , nami nitawapumzisha”.

Baba Mtakatifu amehimiza kwamba , tunapokuwa dhaifu, tunapokuwa hatuna uwezo, tusikate tamaa bali tuwe na imani katika uaminifu na huruma ya Mungu; tumwendee  Yesu kwa ajili ya kuupata msaada wake wa kipekee.   

Papa alieleza na kutafakari  utendaji wa mahujaji wengi katika Mwaka huu wa Jubilee ya Huruma, mahujaji toka duniani kote , ambao wanatafuta kupita kupita katika vizingiti vya Mlango Mtakatifu wa Huruma, wakitafuta  msaada na wokovu wa Bwana wa maisha.  SAmesema kuwa,wengi wanaiendea  huruma ya Bwana isiyokuwa na kipimo. Na katika kufanya hivyo wanagundua  kwamba, nira ya Yesu ni nyepesi , kwa kuwa Yesu hubeba  mizigo mizigo ya dhambi za binadamu , na kwa mateso aliyopitia katika ubinadamu wake, ameionyesha  njia ya wokovu, kwamba ni njia iliyojaa miba na mateso.

Baba Mtakatifu ameendelea kueleza juu ya kushiriki  katika mateso ya Yesu akisema kuwa, kwa kuyashiriki mateso tunaweza tambua mapenzi ya Mungu juu yetu, na hivyo kupata uwezo wa kutambua  faraja za kweli  ndani yake, na katika kuushiriki  mpango wake wa wokovu.

Kwa maelezo hayo, Papa aliongeza , hivyo Yesu anatualika sote, pia  kujifunza kumuiga katika kuwahudumia maskini na wa wote wanaoteseka.  Amemsihi kila mmoja wakati wote kutochoka au  kukata tamaa na kuondoa  woga katika kujenga  matumaini mpya kwa Yesu, kwa kuwa Yesu kamwe hamtelekezi mtu.  Hivyo sote na tumwendee Kristo , tukiwa tumejawa na  imani kwake , kama mkombozi pekee, tukijipumzisha ndani yake na kufurahia  kumtumikia.

Baada ya Katekesi alitoa  baraka zake za kitume akionyesha matumaini yake pia kwamba, katika  Sikukuu ya  kutukuzwa kwa Msalaba, bila shaka kila mmoja ameweza kuamusha hisia mpya katika maisha ya kumfuata  Yesu. 








All the contents on this site are copyrighted ©.