2016-09-03 14:42:00

Papa akutana na wafanyakazi wa upendo katika Jubilee ya wahudumu wa kujitolea


(Vatican Radio) Jumamosi asubuhi katika  Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro Vatican, ,  kuliunguruma, ngoma , nyimbo, vigelegele na vifijo, kutoka  kwa maelfu ya wafanyakazi wa kujitolea na wahudumu  wanaofanyakazi katika taasisi za misaada, waliomiminika katika Uwanja wa Kanisa Kuu hili, kwa ajili ya kuadhimisha  Jubilee yao maalum ya mwaka wa Huruma.  

Pamoja na nyimbo na ngoma, pia shuhuda nyingi zilitolewa na watu wa kujitolea wa pande mbalimbali za dunia.

Papa Francisko , akishiriki sherehe hizi ,  katika hotuba yake , alizungumza juu ya mandhari ya upendo,  akilenga katika  aya  za Mtume Paulo, alimoandika juu ya upendo kwamba, hata kama nikinena kwa lugha za malaika , lakini kama sina upendo mimi  nimekuwa kama sauti ya debe tupu au kengele. Hata kama nina kipaji cha kutangaza ujumbe wa Neno la Mungu na kujua kila siri zote  au kuwa na uwezo na imani kali hata ya kuhamisha milima , lakini kama sina upendo mimi  ni kitu bure …

Baba Mtakatifu alitafakari na  kusisitiza kwamba , mafundisho haya yanaonyesha kwa uthabiti wa hakika  katika imani ya  mtu  isiyoyumba . Na kwamba   kamwe upendo wa Mungu hautakiwa kunyauka katika  maisha ya muumini na  katika historia yake.  Upendo wa Mungu daima lazima ujitokeza upya katika utendaji wote wa kazi , na nguvu zote na katika vishawishi vyote  kama matunda ya imani kwa Kristo.

Baba Mtakatifu alisisitiza kwa nguvu Kwamba , Mtume Paulo , anazungumzia  upendo wa kwelli na halisi na  si maigizo au utendaji wa kufikirika usioleweka ,  lakini ni  halisi yenye kuonekana na  kuguswa,  kwa kuwa ni utendaji wa mikono , wenye  kieleleza  halisi kinachoonyesha upendo mkubwa wa  Yesu Mwenyewe. Yesu alionyesha na anaendelea kutuonyesha upendo wa Mungu kwa kufa msalabani.

Katika uso wa ukweli huu, Papa Francis aliongeza kusema kwamba, hatuwezi kukaa kimya au kutojali.  Kanisa  haliwezi kujifanya halioni au kutegea mgongo  aina nyingi za mahangaiko na mateso halisi ya watu hasa watu maskini. Badala yake hujali na kupiga ukelele wa  huruma kwa niaba ya maskini.  Huruma yenye kuonekana katika  utendaji madhubuti , kupitia misaada yake kwa watu wahitaji.

Papa aliendelea kusema kuwa , huruma hii katika ukweli wake,inapaswa kuwa kitambulisho cha kuonekana katika  maisha yetu ya kila siku, ikionyesha wazi utendaji wa Mungu kati yetu. Na kwamba Mkusanyiko huu mkubwa watu wa kujitolea waliofika katika Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, unawakilisha  wahudumu wa upendo na huruma  ya Mungu toka pande zote za dunia.

Papa amewataja wahudumu hawa, kuwa ni watu muhimu na maalum kwa Kanisa , ambao kila siku , katika hali ya kimya kimya, na mara nyingi ,  katika kazi zao za kujitolea, huonyesha  sura ya huruma ya Mungu . Papa aliwahimiza daima kuwa tayari kutoa msaada na mshikamano kwa jamii na waendelee kutenda kazi yao kwa furaha na unyenyekevu . .

Shrehe za maadhimisho hay aya Jubilee ya wahudumu wa upendo ni kama dibaji ya sherehe za  Jumapili tarehe 4 Septemba 2016, ambamo Baba Mtaktifu Francisko ataongoza Ibada ya mIsa kwa nia kumtangaza Mwenye Hei Mama Twreza wa Calcutta kuwa Mtakatifu. Fadhila na upendo wa Mama Tereza wa Calcutta kwa watu maskini zinajulikana duniani kote. Hivyo utendaji wake ni kioo kinacho oneysha cha huruma ya Mungu kwa watu wote bila mipaka. 








All the contents on this site are copyrighted ©.