Masista wa Mtakatifu Xaviery,katika kuikumbuka tarehe 7 Septemba ya 2014,ambamo Masista wenzao watatu waliuawa kikatili wakiwa nchini Burundi na watu wenye silaha kali wasiofahamika, wamekumbukwa na Masista wenzao kwa kuchapisha kitabu chenye jina : "Nenda Kayatolee maisha katika Kazi za Kimisionari." Marehemu Masista hao watatu waliouawa ni Sista Bernadette Boggian, Sista Olga Lucia Raschieri na Sista Lucia Pulici. Inatajwa kwamba , walikuwa wameyatolea maisha yao katika utumishi wa kimisionari barani Afrika.
Katika kumbukumbu ya kupita miaka miwili baada ya mauaji yao licha kwamba bado kuna giza nene juu ya mauaji haya , Alhamis, Septemba 1, 2016, Shirika la Uchapishaji la EMI,lilichapishaji kitabu hicho chenye jina "Nenda, kayatolee maisha , katika kazi za kimisionari, kitabu kilicho jumuisha maoni mbalimbali yaliyotolewa na Masista wanashirika wenzao wanaofanya utume wao nchini Burundi na Congo.
All the contents on this site are copyrighted ©. |