2016-08-16 09:51:00

Papa Kanisa halihitaji urasimu bali huruma


Kanisa halihitaji kuwa na utendaji wenye urasimu kama serikali bali kutumikia kwa upendo nahuruma, katika  kujali  mahitaji ya watu hasa waliosaulika pembezoni katika  umaskini na upweke. Ni  mawaidha ya Baba Mtakatifu Francikso, aliyoyatoa Jumapili iliyopita mchana kabla ya sala ya Malaika wa Bwana ,mbele ya umati mkubwa wa watu waliofika kumsikiliza, tokea  uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu  Petro mjini Vatican. Papa alionya kwamba, waamini wa Kanisa  bila kuwa na mioyo iliyojaa huruma na upendo , kuna hatari kwa kanisa kuwa baridi katika utendaji wake.  Alitaja ubaridi huo  au imani ya uvuguuvugu tu, maana yake , ni kuw ana utendaji  usiyoonyesha dhahiri  utambulisho wa kanisa katika maisha ya kijamii.

Maelezo ya Papa, yalinukuu  maneno ya Yesu ambamo alisema, "Nimekuja kuleta moto duniani na heri ingekuwa  tayari kuna moto mkali”.  Papa Francisko  alisema,  Kristo anataka Roho Mtakatifu kuwasha moto   katika mioyo yetu  wenye kutufanya  kuwa na uwezo wa kutenda  kwa  upendo na huruma.  Moto huu, alielezea, una nguvu katika ubunifu wa kutenda na  hutakasa na kumbadili  kila mwenye  imani kwa Kristo. Ni moto unaochoma  kila aina ya mateso ya kibidamu , kila ubinafsi , kila dhambi, hubadilisha mtu toka ndani na kumfanya upya.  

Papa aliendelea  kufafanua kwamba, , iwapo sisi wenyewe tutajifunua wazi kabisa katika utendaji wa Roho Mtakatifu , tutaweza pata   ujasiri na hamasa  za kutangaza  ujumbe wa Injili  wenye  kufariji , huruma yake na wokovu kwa kila mtu,  ulimwenguni kote, tena kwa  uwazi na bila woga.  Lakini  alionya Papa , moto na hamasa hiyo ni lazima kuanzia ndani ya mioyo yetu.  

Alisistiza kwamba kutekeleza lengo la  Mungu,  Kanisa linahitaji  msaada wa Roho Mtakatifu, kwa  kuwa ndiye mwenye kuondoa hofu na mashaka yote,  na  hivyo  huweza pata nguvu na ujasiri wa  kutembea sehemu zote na katika mipaka yote kwa  usalama. Ili kufanikisha hili, hapahitajiki urasimu wa kiserikali kaitka utendaji wake kwa kuwa kufanya hivyo ni kujihatarisha. 

Badala yake , aliendelea kuzungumzia ushujaa wa kitume ambao moto wake huwashwa na Roho Mtakatifu ndani  ya miaoyo ya watu , moto wenye kusaidia kuvuka kuta na  vikwazo,  na kuleta ubunifu na nguvu za kusonga mbele katika safari ya maisha ya kuelekea mbinguni , safari ambayo barabara yake imejaa  mitego, vishawishi, barabara inayodai  kutoa  hata sadaka ya maisha kwa ajili ya wengine wote. .  

Papa alieleza na kutaja haja ya Mapadre, wote waliowekwa wakfu, na wakristo kwa ujumla , kuwa na hisia hii ya kuwa n hamu ya kuufikia ujumbe wa  upendo na huruma  kwa watu wote,  kwa majirani walio  karibu na walio mbali hasa kwa  wale walio katika mateso ,  umasikini na wote wanaoishi katika hali za wasiwasi  mwingi kutokana na changamoto za maisha ya kibinadamu , kama  wakimbizi .

Papa alieleza hili na kutoa mfano wa Mapadre  na watawa wanaume na wanawake, na walei , waliokwenda sehemu mbalimbali za dunia kwa nia ya kutangaza injili kwa upendo mkubwa na uaminifu, wakati mwingine hata kwa gharama ya maisha yao wenyewe. Papa ameutaja kuwa ni ushuhuda unaopaswa kuzingatiwa na kuigwa maana ni mfano unaotukumbusha kwamba, Kanisa halihitaji utendaji wenye urasimu kama serikali bali ni watu wanaotenda kwa huruma toka mioyo mwao ,kuwa wapelekaji wa neno la  faraja ambalo ni Yesu mwenyewe  kwa watu wote.

Huo ndiyo moto wa Roho Mtakifu.  Kama Kanisa halina moto huo na kama haliruhusu moyo huo kuingia ndani mwake, basi Kanisa hilo ni  baridi. Liko katika hali ya uvuguvugu tu bila kuwa na uwezo wa kutoa  miali ya mwanga  wa maisha ya kweli ya Kristo.  Hivyo Papa alikamilisha hotuba yake kwa kutoa wito kwa wote  kujitafakari iwapo mioyo yao ina uwezo wa  kupokea moto huu.

Na aliomba msaada wa maombezi ya Mama Bikira Mari, ili i Moto wa Roho Mtakatifu uweze kuingia katika mioyo ya Wakristo.  Na pia alikumbusha  Jumapili ilikuwa Sikukuu ya Mtakatifu  Maximilian Kolbe, shahidi wa upendo, akisema  mfano utakatifu wake,   unatufundisha kukumbatia "moto wa upendo kwa Mungu na jirani.








All the contents on this site are copyrighted ©.