Sisi sote tunahitaji faraja kutoka kwa Mungu, upendo wa Bwana usioweza kuondolewa kwa wote wanaomridhia. Ni maelezo ya Papa Francisko, Alhamisi jioni,wakati akiongoza mkesha wa maombi katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, kama sehemu ya maadhmisho ya Siku Kuu ya Kupaa Rabbi. Mkesha huo uliongozwa chini ya jina” kufuta Machozi"kwa nia ya kuwafariji wale wote walio katika hali za mateso. Katika Mkesha huu,mmoja wa Wanafamilia waliokabiliwa na mateso katika maisha yao , alitoa ushuhudu wake juu ya uchungu wa maisha waliyoyapitia na jinsi walivyosaidiwa kupunguza uchungu huo. Aidha wakati wa Maombi haya , kulionyesha masalia ya Mama yetu wa Machozi wa Siracuse. Masalia hayo yanahusiana na muujiza uliotokea mwaka 1953, wakati picha ndogo ya Moyo safi wa Maria, iliiyokuwa imetundikwa juu ya Kitanda cha Wanandoa vijana Waitaliano, ilitoa machozi ya uchungu.
Baba Mtakatifu Francisko katika tafakari yake , kwa ujumla aliwatia moyo wote wenye uchungu na mateso , kwamba hawako peke yao, iwapo watazamisha mateso na uchungu wao katika sala na tumaini kwamba Yesu na Maria wako karibu nao daima. Papa alionyesha kutambua wazi kwamba nyakati za huzuni, mateso na ugonjwa, huwa ni wakati wa uchungu wa mateso na huzuni zinazotoka moyoni , ni wakati ambamo mtu huhitaji kupata neno la faraja , neno la kumfuta machozi yake. Huu ni wakati ambapo tunahitaji ukaribu wa mtu mwingine, walau kupata hisia za huruma ya wengine kwamba wanajali. Papa alieleza na kusema bila shaka kila mmoja amewahi kuguswa na wakati mgumu wa kuhuzunisha , wakati wa wasiwasi na kuvunjika moyo kwa yalie yaliyotokea , kuona kama hakuna tena matumaini kwa nyakati zijazo. Na kwamba, hali hii ya uchungu na mateso, inaweza kumpata mtu yeyote na wakati wowote. Kwa hiyo ni muhimu na vyema kwa kila mmoja kuwa tayari kuelewa uchungu na mateso ya wengine na kuwa tayari kutoa msaada na faraja hata kama ukaribu huo hautoi jawabu kamili la kutatua tatizo lakini husaidia kupunguza uchungu moyoni.
Papa alieleza na kutazama kwa kina hali za nyakati hizi akisema ni nyuso ngapi zenye huzuni tunazoziona kwa watu wengi wanaotuzunguka pande zote? Watu wanaotokwa na machozi mengi, machozi yanayomwagika juu ya uso wa dunia kila siku , kutokana na sababu mbalimbali , na kutangeneza bahari ya majonzi inayolilia huruma, huba na faraja. Na alibalini kwamba, machozi yenye uchungu zaidi ni yale yanayosababishwa na ukatili wa binadamu, asiyekuwa na huruma, mwenye kuchinja wengine mbele ya jamii, familia, watoto , baba na mama. Ni uchungu gani wanaoupata wanafamilia hawa, Papa alihoji kwa masikitiko.Watu kama hao hukeshi wakilia tangu mapambazuko hadi machweo ya jua na usiku mzima.Kwao inakuwa vigumu kuona mapambazuko ya siku mpya.
Kwa uwepo wa mateso kama hayo, Papa anasema, sote tunahitaji kuwa na moyo wa huruma na kuwapa wanaoteseka faraja za kweli zinazotoka kwa Bwana . Sisi sote tunaitwa kufanya hivyo. Tunahitaji kuwakaribia na kupagusa machozi yao kwa huruma yake Yeye Bwana atakayekuja kufuta machozi yetu wote.
Papa aliendelea kutoa neno la faraja na kuwatia moyo wote akisema , katika mateso na huzuni zetu hatuko peke yetu. Bwana wetu Yesu Kristo tunaye mwamini anajua nini maana ya mateso na uchungu wa kulia, kwa kuwa aliyapitia mateso haya katika maisha yake ya kibindamu. Na hivyo, Mama Kanisa anatuhimiza kusonga mbele na hija ya maisha kama ilivyokuwa Yesu, alimwona Maria akitoa machozi kwa kifo cha ndugu yake Lazaro. Wala hakuweza kujizuia kutoa machozi. Alikuwa amezongwana uchungu wa ndani na kuanza kulia( Yn 11: 33-35). Maelezo ya Mwinjilisti Yohana, yanalenga kutoonyesha kwa kiasi gani Yesu alishiriki katika huzuni na majonzi ya rafiki zake. Hili linatupa faraja kwamba wakati wa Uchungu na kulia Yesu anatujali, yu karibu nasi akitufariji. Yesu ana uzoefu katika nafsi yake mwenyewe, hofu ya mateso na kifo, hamu na kuvunjika moyo katika usaliti wa Yuda na Petro alipomkana, maumivu aliyoyapata kama ilivyokuwa wakati alipompoteza rafiki yake Lazaro.
Papa alieleza na kuongeza wakati wa machafuko, huzuni na uchungu wa kutoa machozi, moyo wa Kristo uliotolea sala kwa Mungu Baba, maombi hayo yanakuwa ni dawa ya kweli kwa mateso mateso yake . Katika sala, sisi pia tunaweza kuhisi uwepo wa Mungu. Huruma yake inayoonekana katika macho yake, yenye kutufariji na kutupa nguvu mpya katika kutumaini . Papa alitoa wito na tuwe kama Yesu, alivyosimama mbele ya kaburi la Lazaro, na kuomba akisema: "Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia. Nilijua kuwa unanisikiliza daima "(Yn 11: 41-42). Na ndivyo sisi pia tunahitaji kuomba kwa uhakika kwa Baba,tukiwa na imani kamili kwamba anatusikiliza, kwa maana upendo wa Mungu, ulio miminwa mioyoni mwetu, unaturuhusu sisi kumwomba Baba Yetu wa mbinguni na hakuna Mtu anayeweza kumtenga mbali na wanaompenda, kama Mtume Paulo anavyoleza "Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je ni ugumu wa maisha, au dhiki, au mateso, au njaa, au uchi au upanga? ... Lakini, katika mambo hayo yote tunashinda zaidi ya kushinda kupitia kwa yeye aliyetupenda.
Papa alieleza na kuonyesha imani yake kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala watawala, wala yaliyopo, wala mambo yajayo, wala wenye uwezo, wala ya juu au yaliyo chini, wala kitu kingine chochote katika viumbe wote, hayatakuwa na uwezo wa kututenga na upendo wa Mungu katika Kristo Yesu Bwana. Na kwamba katika mguu wa msalaba, Mama wa Yesu, daima huko hapo tayari kutufuta machozi yetu. Kwa mkono wake ulionyoshwa, yeye hutusaidia kuinuka na yeye huambatana nasi katika njia ya matumaini, alimalizia Papa.
All the contents on this site are copyrighted ©. |