2016-04-20 15:37:00

Katekesi ya Papa yadai Mkristo kutambua tofauti kati ya dhambi na mdhambi


Baba Mtakatifu Francisko, akiendelea na  mfululizo wa mafundisho  yake juu ya huruma ya Mungu  katika kipindi hiki cha Jubilee ya Mwaka Mtakatifu wa Huruma,  Katekesi yake kwa Mahujaji na wageni,  Jumatano hii, imevuviwa na Injili ya Luka ,mnamo onyesha huruma ya Mungu kwa mwanamke mdhambi aliyeingia nyumbani kwa  Mfarisayo aitwaye Simoni. Mwanamke aliyejulikana kama mdhambi, anaingia nyumbani kwa Simoni na kuaguka miguuni pa Yesu na kuugua kilio kwa machozi mengi  aliyoyakausha kwa nywele zake na kuibusubusu miguu ya Yesu na kuipaka mafuta ya marhamu ya bei ya juu.

Papa amelitafakari tukio hili akisema , akisema mna sura mbili, sura ya  kwanza,  unafiki wa Simoni  Mwandishi na Mwanasheria,  anayetazama dhambi za wengine na kuhukumu . Sura ya pili ni ya mwanamke, mdhambi anayeonyesha moyo wa majuto na unyenyekevu wa mtu mdhambi. Wakati  Simoni anamhukumu mwanamke kwa matendo yake,  licha ya kuwa mwenyeji  wa Yesu, yeye  hakuwa na wazo la  kujipatanisha zaidi na Yesu au kuyashiriki maisha ya Bwana wake. Lakini  mwanamke, anatenda kinyume,  yeyé anaonyesha kujutia matendo yake , anaionyesha hali yake ya ndani kwa uwazi na kumwomba Yesu ayabadilishe maisha yake . NMwanamke anaonyesha imani yake kubwa kwa Yesu,  upendo wa kweli na kamilifu na unyenyekevu, uliogusa huruma ya Mungu na kusamehewa dhambi zake.

Papa Francisko aliendelea kufafanua kwamba, Yesu hakunyanyapaa mwanamke mdhambi  kwa  kuwa alitofautisha kati ya dhambi na mdhambi.  Hili linakuwa ni fundisho kwa Simon na sisi sote kwamba,  hatupaswi kuwatenga wengine  kwa sababu ya dhambi zao, kwa kuwa huruma ya Mungu hutolewa kwa watu wote wanaojutia dhambi zao  na kuwa na imani kwa Mungu kama ilivyokuwa kwa mwanamke, kwa majuto na imani yake alisamehewa  kusamehewa dhambi zake.

Papa alieleza na kuonya kuwa , tabia ya Simoni   Mfarisayo, pia  ipo kwetu . Daima tunataka kujiweka mbali na wadhambi ili tusije ambukizwa nao. Tuna wanyanyapaa wengine eti kwa sababu ni wadhambi. Lakini Yesu anamfundisha Simoni  kutenda kinyume na mawazo hayo.  Yesu anatufundisha  kutofautisha kati ya dhambi na Mdhambi . Na kwamba hatupaswi kuikubali dhambi, lakini twaweza kuwa karibu na  wenye dhambi, hasa  kwa kuwa sisi sote ni wadhambi mbele ya Mungu.  Sisi sote ni kama wagonjwa,  tunaohitaji  kuponywa na ili tupate kutibiwa kwanza  tunahitaji kutambua  maradhi yetu na kumweleza daktari.  Tunahitaji kukutana na  daktari wa Roho ambaye ni Yesu .   

Yesu  aliye Mtakatifu na Mungu, kwa huruma yake hakumzuia mwanamke mdhambi kujieleza  kwa matendo. Anakubali kuguswa na mdhambi bila kumzuia au kuonyesha hofu ya kuchafuliwa nae. Yesu aliguswa na mwanamke akiwa huru kabisa , kwa sababu yu karibu na Mungu ambaye ni Baba mwenye Huruma.  Katika ukaribu huu na Mungu, Baba mwenye huruma nyingi, Yesu anatufundisha  kuwapokea wadhambi kama hatua ya kwanza ya kusamehe na kujenga uhusiano mzuri na wengine badala ya kwuatenga mbali kama wakosefu. .  Yesu alimwambia wmanamke "Umesamehewa dhambi zako" na hivyo .. mwanamke akaenda kwa  amani. Bwana aliona usafi wa imani yake na anamwokoa na kutangaza  mbele ya wote: "Imani yako imekuokoa" (mstari 50)..na hivyo kuwa tofauti na  unafiki wa mwanasheria, anaye mhukumu mdhambi . Kwa mwanamke tunaona jinsi dhamiri  yake safi, unyenyekevu na imani vinavyompa hadhi ya kusamehewa  kwa huruma.

Papa alieleza na kuonya kwamba , ndivyo ilivyo kwetu sisi, wote ni wenye dhambi, lakini mara nyingi tunaanguka katika majaribu ya  kuwa wanafiki, kujiona sisi ni bora kuliko wengine.  Hatupaswi kuangalia dhambi za wengine ili kutazama dhambi zetu wenyewe . Kutazama  maporomoko yetu, makosa yetu na kumlilia Bwana.  Somo hili la Injili lenye aya za  wokovu zinatuonyesha jinsi ya kujenga  uhusiano kati ya "mimI" mwenye dhambi na Bwana. Kama Mtakatifu Paulo anavyotukumbusha: "Katika Kristo, kwa damu yake, tunao ukombozi, msamaha wa dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.  Papa ameitaja kuwa ni zawadi ya imani, na hivyo tunapaswa kumshukuru  Bwana kwa upendo wake mkuu  ambao hatuna mastahili ya kuupata. Tunapaswa kushukuru kwa upendo huu uliomwangwa kwetu,  juu ya ndugu zetu, katika nyumba zetu, katika familia zetu na , katika jamii , ambayo ni  huruma yote ya  Mungu kwetu.








All the contents on this site are copyrighted ©.