2016-04-14 12:29:00

Baraza la Umoja wa Mataifa katika mbio za kuchagua Katibu Mkuu mpya


Baraza la Umoja wa Mataifa limeanza Mchakato wa kuchagua Katibu Mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa, kwa kusikiliza maoni na utetezi wa wagombea kiti hicho  kinacho  achwa wazi na Bwana Ban Ki moon anayemaliza muda wake mwishoni mwa mwaka huu. Taarifa ya Alhamsi imetaja uwepo wa wagombea tisa wa kiti hicho wanne wakiwa wanawake na watano wanaume. Majina ya wagombea ni :

 Bi Vesna Pusic wa Croatia  ambaye kwa wakati huu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na masuala ya Ulaya, na anagombea kwa tiketi ya nchi za Ulaya Mashariki. 

Bwana Srgian Kerim wa Macedonia anagombea kwa tiketi ya nchi za Ulaya Mashariki

Bi Natalia Gherman wa Moldova ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano katika Umoja wa Ulaya anagombea kwa tiketi ya Nchi za Ulaya Mashariki  EEG.

Bwana Igor Luksic wa  Montenegro  ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje, anagombea  kwa tiketi ya EEG

Bi Helen Clack wa New Zealand  ambaye kwa wakati huu ni  Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Mipango ya Maendeleo(UNDP) anagombea kwa tiketi ya Ulaya Magharibi. 

Bwana Antonio Guterres wa Ureno  Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Wakimbizi(UNHCR) anagombea kwa tiketi ya Ulaya Magharibi. 

Vuk Jeremio wa Serbia anagombea kwa tiketi ya Ulaya Mashariki 

Danilo Turko wa Slovania kwa Tiketi ya Nchi za Mashariki (

Jumatano Danilo Turko, alitoa  maoni yake juu ya uongozi wa Umoja wa Mataifa katika miaka mitano ijayo  baada ya Ban, akisisitiza umuhimu wa kuimarisha ubia baina ya Umoja wa Mataifa na jumuiya za kikanda, asasi za kiraia, wafanya biashara, na vyombo vya habari ikienda sanjari na Kazi kuu tatu za Umoja wa Mataifa ambazo ni kudumisha amani na usalama, maendeleo endelevu na haki za binadamu.

Aidha Jumatano Mgombea  Dkt. Vesna Pusić, alitoa maoni yaliyojikita zaidi katika usimamizi wa Malengo ya Umoja wa Mataifa. Alisema  Umoja wa Mataifa usipofanya kazi nzuri ya kusimamia  amani, maendeleo, misaada ya  kibinadamu, haki za binadamu, miradi yote ya elimu na maendeleo, yote yatabaki kuwa ndoto tu za kufikirika .  Ni lazima kuwa na usimamizi thabiti wenye kuhakikisha maamuzi yanayotolewa kweli yanatimizwa na nchi wanachama wa umoja huo.

Na  Bi Natalia Gherman, kutoka Jamhuri ya Moldova,pia alitoa maoni yake , na alikazia  zaidi suala la usalama, maendeleo na haki za binadamu, akisema "Hakuna usalama bila maendeleo, na hakuna maendeleo bila usalama, na hakuna lolote bila kuheshimu haki za binadamu. Na Umoja wa Mataifa ni lazima ujitahidi zaidi  kutimiza ahadi zake juu ya  ubia mpya wa kimataifa kwa  manufaa ya wakazi wote wa dunia.  Ni jukumu la Umoja wa Mataifa, kusaidia nchi wanachama kutimiza ahadi hizi. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Alhamisi limeendelea kuwasikiliza wagombea. 








All the contents on this site are copyrighted ©.