2016-03-08 15:02:00

Mkutano wa Bodi ya Ushauri ya Mfuko wa Yohane Paulo II


Kwa muda wa siku tano tangu Machi 07-11 mjini Dakar  Senegal  kunafanyika mkutano wa mwaka wa Bodi ya Wakurugenzi wa  Taasisi ya Yohana Paulo II kwa ajili ya nchi za Ukanda wa Sahel ( Burkina Faso, Cape Verde, Niger, Chad, Senegal, Mali, Guinea  Bissau, Mauritania na Gambia ). Bodi iliyoanzishwa tangu  mwaka 1984 na Mtakatifu Yohane  Paulo II, kama mkono wa Baraza la Kipapa linaloratibu misaada ya Kanisa Katoliki kwa ajili katika kukidhi mahitaji yalazima kwa watu wahitaji wa Ukanda wa Sahel

Baadhi ya Wajumbe wa Bodi hii ni  Askofu Sanou Lucas Kalfa,  wa Banfora (Burkina Faso), Mwenyekiti wa Bodi; Askofu  Paul Abel Mamba, wa Ziguinchor (Senegal), Makamu Mwenyekiti;Askofu  Martin Albert Happe,  wa Nouakchott (Mauritania), mweka hazina; Askofu  Ambroise Ouedraogo, wa Maradi (Niger).;  Muadhama Kardinali  Arlindo Gomes Furtado, Askofu Mkuu wa Santiago ya Cape Verde (Cape Verde), Askofu  Djitangar Edmond,  wa Sarh (Chad);  Askofu  Elison Robert Patrick wa Banjul (Gambia);  Askofu  Pedro Carlos Zilli, wa Bafata (Guinea Bissau); Askofu  Augustin Traore,  wa Segou (Mali).

Katika mkutano huu,  pia anashiriki Katibu mkuu wa Cor Unum, Padre  Giampietro Dal Toso, kama Mtazamaji wa Jimbo la Takatifu. Mkutano kati ya mengine pia  unafanya mapitio katika miradi iliyopendekezwa inayosubiri kupata fedha . Kwa mwaka 2015 jumla ya miradi 91 miradi ilipata ufadhili kwa gharama ya karibu $  milioni 1.

Taasisi hii hufanikishwa kwa ushirikianao na Baraza la Maaskofu la Italia, Baraza la Maaskofu la Ujerumani,  na makanisa na jumuiya  za kijamii, ambazo hutoa msaada  kwa niaba ya Baba Mtakatifu kwa ajili ya jamii  inayoishi katika mkoa huo wa sahel . Lengo la juhudi hizi hasa ni  kupambana na kuenea kwa jangwa. N a hivyo miradi mingi inahusiana na  sekta ya mazingira, usimamizi na maendeleo ya kitengo cha  kilimo, mifumo ya kusukuma maji, uboreshaji wa maji ya kunywa, na nishati mbadala. Pia ina lengo la kutoa mafunzo  ya ufundi , ili waweze kujitosheleza wenyewe kihuduma.  Aidha taasisi hii imekuwa ni chombo muhimu katika ufanikishaji wa mazungumzano baina ya dini walengwa hasa wakiwa waumini wa dini ya Kiislamu.

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu kwa 2015, ambayo kila mwaka hutoa orodha ya maendeleo ya binadamu kwa kila nchi kutoka jumuiya ya kimataifa, ilionyesha kuwa miongoni mwa nchi 20 zilizo chini katika orodha hiyo, 17 za Kusini mwa dunia, saba za  mwisho 7 ni kutoka eneo  mkoa wa Sahel, ambazo ni miongoni mwa mikoa maskini  duniani. Inakadiriwa,  Sahel yenye kuwa na  jumla ya watu milioni 100,kati yao  milioni 24 huishi katika hali umaskini uliokithiri na hasa lishe duni inayosababisha  watoto milioni 6 wenye umri chini ya  miaka 5 kukabiliwa na utapiamlo. Moja ya matatizo makuu  yanayosababisha hali hiyo ni kupungua kwa maliasili: kwa mfano, Ziwa Chad, ambalo huunganisha mipaka Nigeria, Cameroon, Niger na Chad  likiwa pia na aridhi inayowalisha watu zaidi ya  milioni 2.5,  limepungua kwa karibia asilimia  80% ikilinganishw ana lilivyokuw aktika miaka ya hamsini.  Aidha eneo hilo limekuwa na matatizo makubwa ya makundo ya  ugaidi na utekaji nyara, na hivyo kulifanya eneo hilo  kuwa mahali pa hatari kwa maisha ya kawaida

Hadi mwaka 2014, jumla ya miradi 3100 ilifadhiliwa na Mfuko wa Yohane Paul II ukitumia  zaidi ya $ 36 milioni zilizotengwa, kwa ajili ya Ukanda wa Sahel.








All the contents on this site are copyrighted ©.