2016-02-27 14:20:00

Marehemu Mama Miriam Woldu!


Padre Federico Lombardi, SJ, Msemaji mkuu wa Vatican anasema, Baba Mtakatifu Francisko amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mama Miriam Woldu, aliyekuwa anafanya kazi kwenye Hosteli ya Mtakatifu Martha, ambako Baba Mtakatifu Francisko anaishi kwa sasa. Ibada ya mazishi ya Marehemu Mama Woldu imeadhimishwa Jumamosi, tarehe 27 Februari 2016 kwenye Kanisa la Mtakatifu Stefano lililoko mjini Vatican.

Kabla ya Ibada ya Misa Takatifu, Baba Mtakatifu Francisko alikwenda Kanisani hapo kutoa heshima zake za mwisho kwa Marehemu Miriam Woldu na kusali kwa kitambo kwa ajili ya kuombea roho ya marehemu Woldu, ambaye hivi karibuni alikutwa amefariki dunia nyumbani kwake. Baba Mtakatifu mara baada ya sala, ameweka shada la maua na baadaye kuondoka.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.








All the contents on this site are copyrighted ©.