2016-02-23 14:53:00

Papa : Ukristo ni ukweli na si unafiki


Baba Mtakatifu , Jumanne akihubiri katika Kanisa ndogo la Mtakatifu Marta, ndani ya Vatican , amesema Ukristo ni kutenda  mema na si porojo za kinafiki na  ubatili. Pia ameasa kwamba,  wakati huu wa  Kwaresima, hutukumbusha njia inayofaa kutembea  katika maisha . 

Homilia Baba Mtakatifu Francisko,  imekemea tabia  ya unafiki, kujionyesha kwa maneno kama ni mtu wa dini, lakini kumbe kimatendo ni mbali na dini. Aliendelea kuyazungumzia maisha thabiti ya Mkristo, kwamba humwonyesha  Mungu wa kweli. Na akaonya Wakristo wanaoishi kinyume na maisha hayo, ambao kinafiki hujionyesha kama ni Wakristo safi lakini  kumbe  kimaisha utendaji wao uko  mbali na Ukristo. Ametaja unafiki huo  hulidhoofisha kanisa, kwa kuwa,  wasio Wakristo hawezi ona ukweli wa Ukristo na hivyo hujiweka mbali. Aliendelea kueleza juu ya Wakristo wanafiki ambao hutenda kwa ufahali na majivuno ya maneno  badala ya kutenda kwa unyenyekevu, kuwajali wahitaji na maskini zaidi.

Tafakari ya Papa , ililenga kufafanua aya za Liturujia ya Neno la Siku, ambamo  nabii Isaya na  Injili ya Mathayo, kwa mara nyingine  wanaeleza  kinachotakiwa kufanywa na muumini Mkristo. Papa Francisko alikazia zaidi maneno ya Yesu,  ambamo ameuzungumizia  unafiki wa Waandishi na Mafarisayo,na kuwataka  wanafunzi  wake  na umati wa watu waliokuwa wakimsikiliza,  kuyachukua yale wanayofundisha walimu hao na si  kuiga matendo yao.  

Papa alieleza na kutaja uzoefu wake  akisema ni mara ngapi tunasikia mtu akijigamba kuwa Mkatoliki safi , lakini hata hajua kwa wakati huo Kanisa liko ktiak kipindi gani na linafanya nini , au mara ngapi wazazi husema  wao ni Katoliki lakini hawana hata muda wa kuzungumza na watoto wao juu ya maisha ya Mkatoliki yanavyo paswa kuwa.  Aidha alitoa mfano wa watu wanaopeleka wazazi wao katika nyumba za wazee na kuwatelekeza huko, badala ya kuishi nao.

Papa mara kwa mara  pia  alirejea maneno ya Isaya, yenye kuonyesha kile Mungu anachotaka  kwa biandamu  kwamba hasa ni kuachana na  matendo maovu, badala yake ajifunze kuw amtu mwema .  Ni kuacha na  dhuluma  na kutenda kwa haki .  Ni kutetea yatima na wajane wanaonewa na si kuwagandamiza.  Ni kuwaonyesha wengine huruma ya Mungu isiyokuwa na mwisho  kwa  binadamu, Mungu anayetoa mwaliko daima wa kuingia katika mazungumzo nao  hata kwa mwenye dhambi nyingi, yeyé atazitakasa na kuzifanya kuwa nyeupe kama  heluji .

Hiyo ndiyo huruma ya Mungu ambayo hutolewa kwa wale wanaopenda kukutana naye  katika majadiliano ya kweli , kuhusu mambo ya kufanya na yale yasiyofaa .  Huu ni upendo mkubwa wa Bwana kati ya kusema na kutenda.  Kuwa Mkristo ina maana ya kutenda. Kufanya mapenzi ya Mungu kila siku  hadi siku ya mwisho, ambapo Bwana atarejea na kuuliza ulifanya nini kwa ajili yangu?  

Baba Mtakatifu alikamilisha homilii ayake kwa kuomba hekima za Bwana, zituwezeshe  kuelewa  tofauti kati ya kusema na kutenda , zitufundishe njia ya kufanya na kutusaidia kutembea katika  barabara ya wema na huruma kimatendo , kwa sababu barabara ya maneno bila vitendo ni sawa na barabara waliyotembea walimu wa sheria na Mafarisayo waliotajwa katiak Injili , ambao walipenda kuhutubia watu kwa maneno , lakini utendaji wao ukiwa mbali na hayo waliyoyahubiri.  Amemwoba Bwana atufundishe  njia  ya Injili. 








All the contents on this site are copyrighted ©.