2016-02-22 10:18:00

Papa atoa zawadi ya dawa ya Kiroho kwa mahujaji na wageni


Kwa ajili ya kipindi hiki cha Kwaresima,Jumapili wakati wa Sala ya Malaika wa Bwana,  Baba Mtakatifu Francisko alitoa kiboksi kidogo cha zawadi ,  kilichotajwa ndani mwake kuwa na dawa ya kiroho  ya Huruma ya Mungu. Dawa hiyo ni Rosare ndogo na Sanamu ya Huruma ya Yesu.

Katika hotuba yake, alikumbusha maana ya kipindi cha kwaresima akisema huu ni wakati kukamilisha safari ya uongofu , ambayo kiini chake ni matendo ya huruma, yenye kuonyesha huruma ya Mungu. Na alimtaka kila mwamini kuipokea zawahi hii kama msaada wake  wa  kiroho, na hasa katika wakati huu wa  Mwaka wa Huruma, waweze kueneza upendo, msamaha, na udugu kati ya Watu.

Hii ilikuwa ni mara ya pili kwa Papa kutoa ishara ya "zawadi ya Huruma ya Mungu" kwa waamini. Mara ya kwanza alifanya hivyo,  Novemba ya 2013, wakati wa kukamilika wa Maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Imani , ambamo aliwataka waamini kutumia "dawa hiyo ya kiroho" kwa ajili ya kuzaa matunda yaliyo  thabiti zaidi ya kiroho kutokana na neema walizozipata wakti wa maadhimisho ya mwaka wa Imani .  Katika matukio yote mawili,  zawadi hii ya Papa , ilisambazwa na wafanyakazi wa kujitolea, kwa watu wote bila kujali hadhi yao , wakiwemo pia watu maskini wasio na makazi, wakimbizi, na maskini wahamiaji. 

Papa: awataka Wakristo kukomesha adhabu ya kifo

Aidha Jumapili iliyopita,  Papa alitoa wito kwa Wakristo na watu wote wenye mapenzi mema ,kutenda kwa ushupavu zaidi, kwa ajili ya  kuhakikisha adhabu ya kifo inafutwa katika uso wa dunia, na hali ya maisha  namzingira katika magereza, vinaboreshwa, kwa kuwa kufungwa hakupotezi heshima ya utu wa mtu. Baba Mtakatifu Francisko alitoa rai hiyo, baada ya sala ya Malaika wa Bwana.

Wito wa Papa ulilenga hasa  kuwataka viongozi wa serikali,waridhie utiaji wa saini katika hati ya makubaliano ya kimataifa, inayotaka kufutwa kwa adhabu ya kifo duniani.  Na  ombi lake liliwalenga  Viongozi  Wakatoliki, akiwataka wawe na ujasiri wa kuwa mfano  katika kukataa  kutekeleza hukumu yoyote ya kifo, na hasa katika mwaka huu Mtakatifu wa Huruma ya Mungu.  Papa alitoa ombi lake akiangalisha katika  mazingira ya uwepo wa Kongamano la Kimataifa  kwa ajili ya kukomesha adhabu ya kifo, Jumatatu hii, kama inavyo hamasishwa na Jumuiya ya Mtakatifu  Egidio,  chini ya Kaulimbiu” Dunia isiyokuwa na  adhabu ya kifo."

Baba Mtakatifu ameonyesha matumaini yake kwamba, kongamano hili, litaweza  kutoa msukumo mpya katika juhudi zinazolenga  kukomesha adhabu ya kifo, juhudi zinazoonekana kupambana na upinzani zaidi ,hata  katika vyombo halali  vya ulinzi jamii. Amesema, jumuia za kisiasa na  kijamii,  zina njia  nyingi zinazoweza  kupambana na uhalifu bila  kumpokonya mhalifu haki yake ya kujirekebisha na kuongoka. Papa aliiweka hoja hii ya adhabu ya kifo katika mtazamo wa mfumo wa mazingira ya kisheria yenye kwenda sambamba na heshima ya mwanadamu katika mpango wa Mungu wa wokovu. Alifanya rejea katika Maandiko Matakatifu, “Amri, 'Usiue', akisema kuwa  amri hiyo ni ya thamani sana, na huwalenga watu wote, wenye hatia na  wasio na , kwamba, kwao wote wana  haki isiyoweza ondoshwa kwao , haki ya kuishi , kama zawadi ya Mungu.








All the contents on this site are copyrighted ©.