2016-02-22 10:02:00

Papa ashukuru Mungu kwa kufanikisha ziara yake Mexico


Jumapili ya Pili  ya kipindi cha kwaresima,  kabla ya sala ya Malaika wa Bwana,  Baba Mtakatifu Francisko , katika tafakari yake fupi kwa mahujaji na wageni,  waliokusanyika katika Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro Vatican,  alitafakari ziara yake ya kitume nchini Mexico.   

Papa  alianisha uzoefu alioupata katika ziara hiyo na yaliyoandikwa katika somo la Injili juu ya tukio la Yesu kubadilika sura  akisema  kuwa , pia wakati wa ziara yake ya Mexico ,  aliweza ona mabadiliko,   kwa Bwana  kumwonyesha  mwanga wa utukufu wake, kwa njia ya mwili wa Kanisa lake, la Watu  Watakatifu wanaoishi katika nchi ya Mexico.

Alirudia kutaja nia ya hija yake Mexico kwamba, ilikuw ani kwenda kuhiji katika Madhabahu ya Mama yetu wa Guadalupe. Kutafakari mbele ya sanamu hiyo ya miujiza,  upendo na huruma ya  Bikira, ambaye mahujaji wengi hufika mbele yake, wakiwa wamejawa  na yote mioyoni mwao , furaha , huzuni na mateso mengi, kutoka bara lote la Amerika,  kwa nia ya  kuomba msaada, tokea  mahali hapo ambapo Bikira huyo wa  Morenita mwenyewe,  alijionyesha kwa  Juan Diego  Mhindi mwekundu, kama mwanzo wa uinjilishaji kwa bara  la Amerika ya Kusini na mwanzo wa ustaarabu mpya kama  matunda ya kukutana kwa tamaduni mbalimbali. "

Papa alitaja hilo kuwa ndiyo urithi wa kweli Mexico walioupokea kutoka Bwana, kudumisha  utajiri wa utofauti, na, wakati huo huo, kudhihirisha umoja  katika  imani moja.  Papa Francis akiw aMexico alisema yuko Mexico, kama ilivyokuwa kwa watangauzlizi wake , kuimarisha imani ya watu Mexico, lakini pia nao kuthibitisha imani yao. Maelezo ya Papa yalilenga katiak ushuhuda uliotolewa na  watu wa  Mexico ikiwa ni familia,  vijana, Mapadre na Watawa, Wafanyakazi na Wafungwa kwamba,  ulikuwa ni ushuhuda wa imani ya wazi na imara, ushuhuda wa imani wanayoiishi,  imani iliyobadilisha maisha yao .

Baada ya malezo hayo , Papa alitoa shukurani zake za dhati kwa  Bwana na kwa Bikira wa Guadalupe, kw akumjalia safari nema na  pia alitoa shukurani zake kwa wale wote waliohusika katika kazi za maandalizi na mipango yote iliyofanikisha ziara yake  Mexico, ambayo ameitaja kwamba imekuwa ya mafanikio.  

Na mwisho alitoa shukurani kwa Utatu Mtakatifu , uliomwezesha kukutana na ndugu yake mpendwa katika Kristo, Patriaki Kirill, Askofu Mkuu wa Kiekumeni wa Moscow na Urusi yote , mkutano uliofanyika Havana Cuba wakati akielekea Mexico.  Na alihitimisha na ombi kwa Mama wa Mungu , aendelee kuwaongoza katika njia ya kutembea pamoja  kwa umoja kamili kama  wafuasi wa Mwana wake Yesu Kristo








All the contents on this site are copyrighted ©.