2016-02-01 13:26:00

Jumuiya ya Kimataifa yahimizwa kusaidia wanaokabiliwa na majanga asilia


 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki moon , Ijumaa iliyopita katika  mkutano wa wahisani  wa kimataifa, uliofanyika  mjini Addis Ababa , aliihimiza  Jumuiya ya kimataifa,  kuunganisha nguvu  na mataifa yanayokabiliwa vibaya na ukame , kwa mfano Ethiopia, hasa katika kukabiliana na majanga asilia kama ukame wa kukithiri, unaosababisha maelfu ya watu kukosa chakula . Bwana Ban alikuwa mjini Addis Ababa kwa ajili ya kushiriki  katika Mkutano wa  26 wa  Umoja wa Afrika.  Ban Ki moon pia alitembelea maeneo yaliyokumbwa vibaya na  ukame  Ethiopia, ukame unaotajwa kuwa  matokeo ya  El Niño  na athari  za mabadiliko ya tabianchi.

Katika mkutano na wahisani ,  Ban alikiri uwepo wa  dharura  nyingi zinazokabili  Serikali  za nchi zinazokumbwa na majanga asilia  kama  El Niño, akionyesha kujali kwamba,  kwa bahati mbaya hali hizo hazitabiliki  asilimia kwa mia.

Alieleza na kupongeza  uongozi wa  serikali ya Ethiopia, kwa jinsi ulivyoweka mkazo  katika kukabiliana na matokeo ya janga hilo la  ukame mpaka sasa.  Na akataja nia za Umoja wa Mataifa,  kwa kushirikiana na Benki ya Dunia, kuunga mkono  Mpango wa serikali, unao wania  kutoa msaada kwa  watu milioni nane, walio katika hatari kubwa za kukabiliwa na   ukosefu wa chakula  na fedha, kutokana na hali ya ukame . .

Aidha KatibuMkuu alisifu juhudi za kimaendeleo zinazofanywa Ethiopia  katika miaka ya hivi karibuni kwamba zinavutia kusaidia taifa hilo, hasa katika uimarishaji na usambazaji wa mitandao ya miundombinu kwa jamii na kwa ajili ya ujenzi wa ujasiri wa kitaifa kwa siku zijazo, kama ilivyokubalika katika Malengo ya Maendeleo  Endelevu , hakuna wa kubakishwa nyuma, iwe katika Pembe ya Afrika au  kwingineko. Katibu Mkuu Ban Ki moon, alieleza akisiema , uwepo wa migogoro na vipeo ni vikwazo vikubwa katika ufanikisha wa Ustawi na maendeleo ya kudumu kwa wote.

 Katibu Mkuu aliweka matumiani yake katika Mkutano wa Dunia juu ya ubinadamu, utakaofanyika  mjini Istanbul tarehe 23 na 24 Mei 2016, kama ni  fursa kwa waliopiga hatua za kwanza katika maendeleo kusaidia waliobakinyuma.  








All the contents on this site are copyrighted ©.