2016-01-29 14:17:00

Papa akutana na wajumbe wa Baraza la Kipapa la Mafundisho tanzu ya Kanisa


Ijumaa hii katika kukamilisha mkutano wake, wajumbe wa Baraza la Kipapa la Mafundisho tanzu ya Kanisa walikutana na  Baba Mtakatifu Francisko  katika ukumbi wa Clementina hapa Vatican. Papa katika hotuba yake, alilenga zaidi  katika mambo matatu; mwingiliano wa uhusiano wa kazi za matendo ya huruma kiroho na kimwili;  umuhimu wa utendaji wa pamoja katika maisha ya kazi na uongozi , na tunu za hirakia ya uongozi katika maisha na utume wa kanisa.

Pamoja na kutoa shukurani zake za dhati kwa watendaji wote wa kazi za shirika hilo na washauri wake, pia Papa ameonyesha matumaini yake kwamba, katika kipindihiki cha Jubilee ya Mwaka Mtakatifu, waamini wote wa Kanisa wataweza kuhuisha upya imani yao kwa Yesu Kristo, ambaye ndiyo sura ya huruma ya Baba, na njia inayo unganisha Mungu na mwanadamu.  Hivyo huruma inakuwa ni msingi wa maisha ya Kanisa yaliyosimikwa katika ukweli wa kwanza wa Kanisa, ambao ni upendo wa Kristo.

Kwa mtazamo huo, Papa alihoji  kwa vipi inaweza kukosekama kwa  Wakristo,  wachungaji na walei,  hamu  ya  kutaka kugundua na kuweka matendo ya huruma kama kiini cha utendaji wote  katika kipindi hiki cha Jubilee,  katika maisha ya kawaida na kiroho pia. Papa ameeleza na kuonya kwamba,  mwisho wa safari hii ya maisha,  tutapaswa kujibu, iwapo tuliweza kulisha na kunywesha wenye  njaa na kiu, sawia kutakuwa na swali jingine iwapo tuliweza kuwasaidia watu kutoka katika hali zao za mashaka na  na kuwapokea wenye  dhambi , kuwaonya au  kurekebisha  mienendo yao,  na  hasa sana katika masuala yanayohusiana na habari za imani ya Kikristo na maisha mazuri.

Hotuba ya Papa iliendelea kurejea kazi msingi iliyokabidhiwa shirika, kueleza kwa ufanisi  upendo na huruma, ambavyo huuunganisha Mungu na binadamu, kupitia Yesu Kristo, ambaye ni  utimilifu wa huruma na upendo wa Mungu, uliotolewa kwa ajili ya wokovu wa watu.  Papa ametaja hiyo ndiyo kazi kuu ya Shirika walilokabidhiwa, na hapo ndipo kuna msingi wake na ukweli wote.  Imani ya Kikristo, kwa kweli, si tu maarifa yaliyohifadhiwa katika nyaraka na vitabu vya kumbukumbu, lakini  ni ukweli  wa kuishi katika upendo. Kwa hiyo, pamoja na mafundisho ya imani, mtu lazima kulinda uadilifu wa maadili, hasa katika mazingira nyeti ya maisha. Mshikamano wa imani  katika nafsi ya utu wa Kristo, ina  maana ya kutoa majibu yote kwa kuzingatia tunu zote za kimaadili.  Kwa mtazamo huo, Papa alitoa shukurani zake kwa wote waliohusika na utoaji wa majibu yanayofaa katika juhudi za kukabiliana na kesi  watoto kutumiwa vibaya na viongozi wabovu wa kanisa.

Papa alieleza na kurudia kuzungumzia umuhimu wa Huduma za kanisa kufanyika kwa  uadilifu wa imani na maadili  kwamba ni muhimu katiak mazingira yote ya kiimani na kanisani . Na kwa kutimiza utume huu, ni muhimu kutenda kazi zote kwa pamoja.   Adiha Papa ametoa shukurani na pongezi zake kwa wale wote wanaotoa mchango wao muhimu kwa Shirika ,  kwa kazi yao nzuri na unyenyekevu , na hivyo amehimiza waendelee  na  moyo huo kama ilivyokuwa katika kushughulikia mada za mkutano wa Shirika uliokamilika..  Papa amesema, kuna haja ya kukuza, katika ngazi zote za maisha ya kanisa, umoja na haki.

Papa ameshauri uwepo wa mikutano kama uliofanyika mwaka jana, uliokutanisha wajumbe kutoka  Mabaraza Katoliki ya Maasskofu ya Ulaya, kujadili kw apamoja  jinsi ya kukabiliana na baadhi ya changamoto dhidi ya Mafundisho na kazi za Kichungaji za Kanisa.  Papa anasema , njia hii inaweza saidia kuinua ari mpya kwa waamiini na umisionari mpya , hasa katiak mataifa ya Ulaya  ambako roho ya ubinadamu inamomonyoka.  Papa ameendelea kulitaka shirika  kuendelea kuimarisha ushirikiano na tume za ushauri kutoka Mabaraza ya  Maaskofu, na pia  Maaskofu kama  mtu binafsi,  pale panapo jitokeza wasiwasi kwa mafundisho ya kweli kutaka kuzonga na malimwengu , na wakati wa madai ya mabadiliko ya haraka, yenye kuongezeka utata katika wa hoja za kiimani. 

Papa pia amezungumzia mchango wao muhimu katika kufanya upya maisha ya kanisa  kupitia  utafiti unaotafuta mkamilishano kati ya tunu za hirakia za utawala na karama. Papa amesema kwa mujibu wa mantiki ya umoja katika tofauti halali - mantiki yenye  kuonyesha sifa  ya kweli katika kila aina ya usharika halisi wa Watu wa Mungu, tunu za uongozi na karama , vimeitwa kufanya kazi pamoja kwa manufaa ya Kanisa na ulimwengu. Ushahuda huu wa kusaidiana, leo hii inakuwa ni hoja ya haraka zaidi kuliko ilivyokuwa kipindi cha nyuma, ikidai kila jumuiya a kanisa, kuonyesha sifa zake  kama kielelezo cha jamii iliyoridhiana, yenye kuishi  katika Kiini cha umoja wa  Utatu wa Mungu na kama zawadi  kutoka kwa  Baba,  Mwana Roho Mtakatifu.  Papa anasema Umoja na wingi ni uthibitisho wa Kanisa ambalo,huongozwa na  Roho Mtakatifu, lenye kutembea  kwa  aminifu  katika  hatua zake zote, kuyaelekea malengo  yaliyowekwa na  Bwana Mfufuka , yenye kuonyesha  mwendo na  historia ya kanisa.  Papa ameeleza na kutoa mfano wa mikutano ya  sinodi ,kama tunda la umoja na ushirikiano  wenye kuongoza katika umoja  halisi  wa kina na mpana zaidi katika huduma ya maisha na utume wa watu wa Mungu . 








All the contents on this site are copyrighted ©.