2016-01-15 14:45:00

Jimbo la Papa halina jawabu la moja kwa moja kupambana na matatizo ya sasa


Askofu Mkuu Janusz Urbanczyk ,  Mwakilishi wa Kudumu wa Jimbo la Papa katika  Shirika kwa ajili ya Usalama na Ushirikiano wa bara la  Ulaya (OSCE),na Mashirika mengine ya Kimataifa yaliyoko mjini Vienna, Alhamis  14 Januari 2016, alitoa mchango wa Jimbo la Papa katika Mkutano wa OSCE  wa 1085,uliofanyika mjini Viena Austria.

Mwalikishi wa Jimbo la Papa, aliuambia Mkutano huo kwamba , mchango wa Jimbo la Papa,  hauna majawabu ya moja kwa moja  yanayweza kutoa  ufumbuzi katika changamoto na hali ngumu zinazoonekana kuvuka mipaka ya uwezo wa dunia kwa wakati huu, lakini linahimiza na kuunga mkono  nia zote zinazolenga kujenga uwanja wa majadiliano, mazungumzano na  mipango mingine inayotafuta  ufumbuzi  uliobora  zaidi, kuliko utumiaji wa mabavu,   kudumisha amani na usalama duniani. Mwakilishi Vatican, alieleza kwa kutazama kwa makini hali ngumu zinazotikisa dunia kama mgogoro wa  uhamiaji , akisema Jimbo Takatifu  mpaka sasa linashukuru kwa  juhudi kubwa za ushirikiano,  unaoonyesha uwepo wa  mshikamano na  maskini wanaotafauta hifadhi na maisha yenye ubinadamu zaidi.

Aidha aliwarejesha washiriki wa mkutano huo, kutazama tatizo jingine linalokabili dunia leo, kuzorota kwa mazingira ya dunia.   Askofu Mkuu Urbańczyk aliuambia mkutano kwa kutaja  hamu  ya Baba Mtakatifu Francisko katika kukabiliana na tatizo hili akiweka matumaini yake kwa  Uenyekiti  wa OSCE  kwamba,  utaweza pitisha hatua mpya  makini na  haraka kwa ajili ya matumizi endelevu ya rasilimali na kuwa na sauti thabiti katika usimamizi wa maliasili, ikiwa ni pamoja na kujaribu kila njia iwezekanavyo,  kukomesha, haraka iwezekanavyo , kwa ubaguzi wa kijamii na kiuchumi katika mifumo yote ya kidunia.

Aidha Askofu Mkuu  Urbańczyk, aligusia  suala la jinsia, aksiema, Baba Mtakatifu Francisko, anasadiki, jinsia   hizi mbili  kiume na kike , tofauti zake , haziondoa  usawa katika kuheshimu ubinadamu wa kila mmoja,  kwa kuwa utofauti katika usawa, ni kirutubisho cha mmoja kwa mwingine, na ni  muhimu kwa ajili ya umoja wa maisha katika jamii, na mwendelezo wa binadamu .  Na kwamba Mwanamke ni ukamilifu wa Mwanamme na mwanamme ni ukamilifu wa mwanamke na uwepo wao hulega kukamilishana, si tu  kimwili,na kisaikolojia,  lakini pia katika mantiki za utu wa binadamu na maisha yake yote.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.