2015-10-23 10:07:00

Papa : bidii zetu zinazohitajika kumfungulia Mlango Roho Mtakatifu


Juhudi zote za Mkristo katika imani ni kwa ajili ya kumkaribisha Roho Mtakatifu moyoni. Ni ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisco wakati wa Ibada ya Misa katika Kanisa ndogo la Mtakatifu Marta hapa Vatican. Papa alisisitiza kwamba, wogofu wa moyo kwa Mkristo , ni utendaji wa kila siku unaoongoza katika njia ya kukutana na Yesu .

Na hivyo kwa Mkristo wogofu ni wajibu. Ni jukumu analopaswa kulifanyia kazi kila siku . Papa alileleza hilo kwa kurejea somo kutoka Kitabu cha Mtakatifu Paulo kwa Warumi ambamo amesisitiza kwamba ili kuondokana na maisha ya dhambi hadi maisha safi Matakatifu ni lazima kuwa na bidii za kufanya hivyo kila siku.

Papa alieleza kwa kurejea Mfano uliotumiwa na Mtakatifu Paulo,  mfano wa mwanamichezo, kwamba hujiandaa mwenyeweili apate ushindi mkubwa. Na ndivyo hata Mkristo anavyotakiwa kujiandaa kila siku kwa ajili ya kuwa mshindi dhidi ya dhambi. Mtakatifu Paulo, Papa alisema "anatuhimiza kusonga mbele na juhudi hizi.

Papa alihoji iwapo huwa tunafikiri kwamba utakatifu huja kupitia juhudi tunazojifanya wenyewe, kama ilivyo kwa mwanariadha anayetafuta ushindi kwa njia ya mafunzo? Ni kweli kwamba juhudi zetu tunazojifanya, katika kazi zetu za kila siku katika kumtumikia Bwana kwa moyo wote, na akili yote na mwili wote ,  pamoja na maisha yetu yote, hufungua mlango kwa Roho Mtakatifu.  Roho Mtakatifu huweza ingia ndani mwetu na kutukomboa! Yeye ni zawadi ya  Yesu Kristo! Vinginevyo, utendaji wetu unakuwa bure.  Juhudi zetu ndizo huweza fungua mlango kwa Roho Mtakatifu.

Baba Mtakatifu alieleza huku akionyesha kutambua kwa jinsi ilivyo vigumu , kutokana na udhaifu wetu , unaotokana na uwepo wa  dhambi ya asili yaani  shetani, ambaye daima, hutuweka katika majaribu ya kuturudisha nyuma, kama  waraka kwa Waebrania , unavyo onya dhidi ya majaribu ya kugeuka nyuma. Unaonya tusirudi nyuma, au kuanguka tena katika dhambi, lakini ni kusonga mbele katika hatua za utakatifu siku hadi siku, hata wakati wa shida na matatizo  makubwa. Papa alieleza na kuhimiza waamini wa Kristo kutafuta  neema za Mungu kwa bidii zote, kama ilivyo kwa mwanamichezo anayepania kupata ushindi mkubwa  katika michezo, hujibidisha katika mafunzo.

Na alionya kwamba baadhi majaribu ni tamaa za uzushi mambo kwa wengine. Kuishinda tamaa hiyo Papa anasema ni kufanya jitihada za  kukaa kimya. Vinginevyo, hatuwezi kuyashinda majaribu, na hivyo tunakuwa dhaifu na kupoteza bidii ya kusali. Lakini pia Papa alisema, mara nyingi ndani mwetu hata tunapo poteza bidii, hubaki mbegu ndogo ya kufanya hivyo. Mbegu hiyo ndogo hutusaidia kutoanguka moja kwa moja chini, au  kurudi nyuma kabisa katika uovu. Lakini huTUsaidia kusonga mbele katika kuielekea zawadi hii, ambayo ni ahadi ya Yesu Kristo, katika haki  ya kukutana naye. Papa alirudia tena , kutoa mwaliko wa kuomba neema hii ya kukutana na Bwana. Kuwa na nguvu, kuwa imara katika mafunzo haya kuelekea kukutana na Bwana wa maisha, hadi kuipokea ile zawadi ya kuhesabiwa haki, zawadi ya  neema, zawadi ya Roho katika Kristo Yesu.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.