Ripoti ya Chama cha Ulinzi wa Mtoto “ kinachojulikana kwa jina la “ suala ya maisha na kifo” inaonyesha kwamba, uzoefu hasi wa utotoni, huathiri maisha yote ya mtu, kitabia na kiafya. Maisha mabaya ya utotoni yanaweza kuwa chanzo cha tabia mbaya za mtu baadaye anapokuwa mtu mzima,na huongeza asilimia kubwa ya vifo vya mapema, myumbo wa maisha, utumiaji wa madawa ya kulevya, kutopenda shule na kuwa na tabia ya hasira na fujo. Yote haya huchangia kuchochea migogoro, na kuendeleza mzunguko wa umaskini na kudumisha ukosefu wa utulivu kwa jamii nzima.
Ripoti hiyo imefanya rejea katika takwimu za Syria zinaonyesha kwamba, wavulana kati ya miaka 13 na 17 wamekuwa na uwezekano mkubwa wa kujeruhi au kuua kwa mara nne zaidi wakilinganishwa na wenzi wao wasichana katika umri huo. Na kwamba uwezekano huu wa kujeruhi au kujeruhiwa wakiwa mbali na wazazi au familia zao , hasa hutokana na matatizo ya kukosa upendo ndani ya familia na msaasa wa kibinadamu kwa watu waliokaribu nao , na hivyo kusababisha matatizo zaidi ya muda mrefu.
Ripoti hiyo inaonya kwamba bila uwepo wa juhudi za kisiasa, na uwezo wa kuhakikisha kwamba, watu wote wanakubalika na ubinadamu wao kuheshimiwa na pande zote zinazopingana, si rahisi kupunguza athari za vita kwenye uwanja wa ubinadamu.
Kwa maoni hayo Ripoti imetaja hatua muhimu za kuchukuliwa kwa ajili ya kujenga moyo wa ubinadamu kwa mtu tangu utotoni kwamba,
• Serikali na taasisi zisizo za kiserikali, wote wanapaswa kujua kanuni za sheria
ya kimataifa ya kibinadamu na jinsi mtu anavyopaswa kuwajibishwa iwapo atapatikana
na hatia ya kukiuka haki za biandamu.
• Vyama vyote vya kisiasa vinapaswa kutoa kipaumbele kwa usalama, ustawi na ulinzi
wa watoto katika hali zote za kidharura.
• Serikali na wafadhili binafsi lazima kukusanya fedha za kutosha kwa ajili ya kuhakikisha
ufanisi katika kazi za ulinzi wa watoto katika hali ya dharura.
• Watendaji wote katika huduma za kibinadamu wanapaswa kushirikiana katika mawasiliano
ili kuhakikisha kuwa mahitaji ya watoto na maoni yao pia yanapewa uzito. .
• Na kwamba watendaji wa huduma ya ubinadamu na wafadhili, kuweka ushiriki wa watoto
katika viituo mkakati kwa ajili ya kuimarisha ushirikiano na watu wazima walioathiriwa
na migogoro, na kutoa tathmini ya mahitaji, na wakati huo huo, kukuza upatikanaji
wa huduma kwa watoto kwa njia za mawasiliano. SOS
Mila Italia imetaarifu.
All the contents on this site are copyrighted ©. |