Homilia ya Papa , wakati wa Ibada ya Misa ya Asubuhi kwa Alhamisi hii, ilitazama kwa makini mateso na mahangaiko mengi yanayokabili watu wa Mungu , akitolea mfano wa mama shujaa katika imani, mama mwenye mme na watoto watatu , mwenye umri chini ya miaka 40 , ambaye anasumbuliwa na maradhi ya mabaya ya kansa yaliyomweka chini kitandani. Aidha alitoa mfano mwingine akihoji kwa nini? Akikumbuka uchungu na mateso ya mama mzee , mtu wa sala na mwamini aminifu kwa Kanisa, ambaye mtoto wake wa kiume pekee aliuawa bila huruma na kikundi cha uhalifu cha mafia.
Kwa nini maovu haya?, sauti ya Papa Francisco ilisikika ikihoji tokea altare ya Kanisa dogo la Mtakatifu Marta Vatican, ambamo alikitazama kwa makini kilio cha Nabii Malaki kama ilivyosikika katika somo la kwanza, akilinganisha na hali halisi za wakati huu.
Alihoji , ni mara ngapi tunaona ukweli huu, watu waovu, watu wabaya ambao wako
mbali na Mungu lakini maisha yao katika mtazamo wa kidunia kwamba, yanawaendea vizuri:
wakionekana kuwa na maisha ya furaha, wana kila kitu wanachotaka, hawakosi chochote.
Kwa nini Bwana anaruhusu hilo? Ni kati ya mlolongo wa maswali yetu yanayotafuta sababu
kwa nini mtu kama huyo asiyejali uwepo wa Mungu, mtu mdhalimu, mwenye kuzua matatizo
mengi kwa wengine mambo yake yote yamwendee vizuri?
Papa alisema, jibu la maswali yetu mengi, limo katika wimbo wa zaburi ya siku , inayotangaza,
Heri mtu yule asiyeketi katika baraza la wadhalimu , Mtu asiyetembea katika njia
za wasio haki na wadhambi lakini mwenye kuifurahia sheria ya Bwana ... Na aliyatumia
maswali hayo yasiyokoma katika moyo wa binadamu wenye tamaa ya kutaka hata ya kuingilia
siri za mpango wa Mungu, katika uhusiano na utendaji wake kwa binadamu, utendaji
wa haki na huruma yake. Papa alirejea maandiko kutoka Kitabu cha Nabii Malaki, ambapo
Bwana anawakemea watu akisema," wewe amenikaidi katika neno, asema Bwana, na bado
wauliza, tumesema nini kibaya dhidi yako?" ' Wewe wasema, ni bure kumtumikia Mungu,na
twapata faida gani kwa kushika amri zake, na kuvaa mavazi toba kwa dhambi zetu, kwa
kumhofia, Bwana wa majeshi?" Wewe mwenye kuwaona waovu na wenye kiburi kuwa ndiyo
wabarikiwa?" Papa Francisko alisema kwa mtazamo wa kidunia , kweli twawaona watenda
maovu kuwa ndiyo wenye mafanikio ambao hata hudiriki kumjaribu Mungu bila woga.
Lakini Papa akaendelea kusema furaha ya watu hao ni ya mpito, maana baada ya maisha
yao hayana nafasi mbinguni maana majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha Enzi,
Papa alieleza na kusema, ni wazi kwa sasa hatuoni matunda ya mateso ya waamini ,
watu wanaoubeba msalaba wao , kama ilivyokuwa kwa Bwana Ijumaa Kuu ya Mateso , lakini
furaha yake ilionekana Usiku wa Jumamosi Takatifu Kuu, matunda ya Mwana wa Mungu
aliye sulubiwa, mateso yake, kufufuka kwa utukufu mkuu. Na ndivyo ilivyo kwa muumini
aminifu ambaye furaha yake imo katika kuzitii sheria za Bwana. Papa amewatia matumaini
wote wanaoteseka na kubaki aminifu kwa Kristo kwamba, kila jambo , litazaa matunda
mazuri. Na kwamba kwa yale yote yanayoonekana kuwa mazuri kwa wadhalimu na waovu,
yatakuwa kama makapi, yatapeperushwa mbali na upepo, kwa sababu Bwana anaijua njia
ya wenye haki, na njia ya wasio itaharibiwa.
All the contents on this site are copyrighted ©. |