Ijumaa 25 Septemba 2015, Baba Mtakatifu Francisko aliutembelea Umoja wa Mataifa na kulihutubia Baraza la Umoja wa Mataifa. Hotuba yake ilisisitiza kwamba, dunia kwa nguvu, inadai serikali zote kuwa na nia na utendaji thabiti, kutekeleza maamuzi yanayotolewa na wote .
Papa Francisco amekuwa ni Papa wa nne kutembelea Umoja wa Mataifa. Na ametembelea kama sehemu ya tukio la Mkutano Mkuu wa 70, na pia kama kumbukumbu ya kupita miaka 50 ya hotuba ya kwanza ya Papa katika Umoja huo, iliyotolewa na Mwenye Heri Papa Paulo VI mwaka 1965. Papa Yohana Paulo II aliutembelea Umoja wa Mataifa mara mbili mwaka 1979 na 1995, na Papa Mstaafu Benedikto XV1 alikwenda mwaka 2008.
Hotuba ya Papa kwa ujumla imetazama umuhimu wa Umoja wa Mataifa, maovu yanayotesa dunia leo hii kama unyonyaji, vita, umaskini, madawa ya kulevya na kutoa wito wa kutafuta jawabu la haraka na fanisi. Papa alisema "napenda kuongeza sauti yangu kwa wale wote wanaotamani, ufumbuzi wa haraka na ufanisi kukabiliana na matatizo haya yanayoirarua dunia".
Katika hotuba hii , iliyopigiwa makofi mara kwa mara , Papa alizungumzia kwa nguvu
zote, haja ya kujenga muafaka imara wenye kuvunja hila zote za utengano na kukosekana
kwa usawa kunako umiza binadamu. Papa alisema ni kuanzia na taasisi za Umoja wa Mataifa
wenyewe, kuwa na sheria thabiti zinazo zingatia sababu za kuanzishwa na kudumisha
mafanikio muhimu ya pamoja kama uboreshaji wa haki za wengi katika neema ya uhuru
na ulinzi wa heshima ya utu mwa mtu. Na aliongeza kusema, "Mafanikio haya yote ni
wanga unaomulika dhidi ya giza la machafuko yanayosababishwa na ulafi, tamaa na ubinafsi
pamoja".
Papa akirejea lengo la kuundwa kwa Umoja wa Mataifa kwamba ni kudumisha haki, aliwakumbuka
wote wale ambao wamekuwa kafara katika utume wao wa kuhudumia ubinadamu wa amani na
maridhiano. Na alimtaja kati ya wengine Mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani na mara
mbili Katibu Mkuu wa UN, hayati Dag Hammarskjold.
Aidha hotuba ya Papa imetaja umuhimu wa Umoja wa Mataifa katika kupambana na na changamoto zinazojitokeza kama vile uhaba wa ruzuku kwa ushiriki nchi na utekelezwaji wa na maamuzi halisi na ya haki. Na pia akazitaka taasisi za Kimataifa za fedha" kuwa macho na "maendeleo endelevu ya nchi"na hasa kujiepusha na maamuzi yenye kukaba koo maoni ya watu mahalia katika kustawisha maendeleo yao,na taratibu za kupambana na umaskini wa kukithiri, kutengwa na utegemezi. Papa alitaja haki kuwa sharti msingi la kufikia udugu mzima uliobora kama kiwango cha juu cha nguvu na thabiti katika dhana ya sheria.
Na kwamba hakuna kundi, mtu binafsi au watu wenye kujiona kuwa na nguvu zote,
wanaoweza kuruhusiwa kukanyaga heshima na haki za watu wengine au makundi ya kijamii.
Na alitazama upande wa mazingira na kusema ukweli wa sheria ya asilia ya mazingira
vizingatiwe kwa sababu, kimsingi binadamu pia ni sehemu ya mazingira na hili linatawaliwa
ina mipaka ya kimaadili, inayotaka hatua za utendaji wa binadamu lazima kutambua
na kuheshimu mazingira. Hivyo haribifu wowote kwa mazingira, ni kuumiza ubinadamu
pia .
Papa anasisitiza kuwa kila kiumbe kina thamani kwa jinsi kilivyo chenyewe na katika
mfumo asili wa kutegemeana na viumbe wengine. Hivyo matumizi mabaya na uharibifu wa
mazingira, inakuwa ni mfumo mbaya wa kutaka kujitenga na wengine, hasa kutokana na
ubinafsi na nguvu ya tamaa za kutaka kuonekana kuwa juu ya wengine na kama matokeo
yake hujenga tabaka la wanyonge na wasiojiweza katika hali za maisha. Utengano kiuchumi
na kijamii, wenye kudhoofisha mshikamano wa jumla wa udugu wa binadamu na hivyo
inakuwa ni shambulio kubwa kwa haki za binadamu na mazingira.
Papa alieleza na kusisitiza kwamba, dunia kwa nguvu inataka serikali zote ziwe
na nia madhubuti na vitendo thabiti. Ni lazima kuhifadhi na kuboresha mazingira li
kuondokana na mijeledi ya kijamii na kiuchumi yenye kujenga utengano, wenye kuathiri
wengi , mijeledi kama ya "usafirishaji haramu wa binadamu", "biashara haramu ya silaha
na madawa, ugaidi na uhalifu wa kupangwa wa kimataifa.
Papa alitoa ombi la kutositisha mchakato wa kutazama hali halisi katika maisha ya
kijamii, ili kuchukua hatua zinazo stahili katika za kukabiliana na wanachopambana
nacho wanaume na wanawake, ambao mara nyingi wanaishi katika umaskini na wenye kupokonywa
haki zao kama binadamu. Ni lazima kuwashirikisha
watu mahalia katika utendaji wa shughuli zote kwa stahili ya hatima yao wenyewe na
katika ushirika na wanadamu wengine.Katika Mshikamano wa maendeleo ya binadamu na
zoezi kamili ya utu wa binadamu lisilo na mbadala. Wakati huo huo - aliendelea - viongozi
lazima kufanya kila linalowezekana ili kila mtu aweza kupata mahitaji yake msingi
ya kihali na kiroho ili kudumisha hadhi ya utu wake na kuunda familia, katika misingi
yake asilia kama kiini cha msingi wa maendeleo yoyote ya kijamii.
Papa ametaja mahitaji matatu katika kiwango msingi cha nyenzo ya utu wa binadamu
kihali kwamba ni kuwa na makazi yaani nyumba ni, kazi na ardhi; na pia anahitaji katika
ngazi ya kiroho: uhuru wa roho, ambao hautangamani na uhuru wa dini, haki ya kupata
elimu na haki nyingine za kiraia . Papa alizungumzia pia juu ya ardhi, kama haki
ya kuishi na haki ya uwepo kwa maumbile yenyewe.
Na kwamba ulinzi wa mazingira na mapambano dhidi ya ubaguzi, unahitaji kutambua sheria
asili ya maadili iliyoandikwa katika maumbile yenyewe ya binadamu, ambayo ni pamoja
na tofauti ya asili kati ya mwanamke na mwanaume (cf .. Msifiwa ndiyo, 155) na heshima
kwa maisha katika hatua zake zote.
Bila ya kutambua asili hii, suala la kupuuzia mipaka ya maadili mipaka - aliendelea
Papa, huleta hatari za mfuko wa vita, dhuluma, rushwa, uendelezaji wa kiitikadi
ukoloni, maisha yasiyo kuwa ya kawaida, yenye kukosa heshima kwa utambulisho a watu
wageni , kukosekana kwa uwajibikaji. Inapaswa kukumbukwa kwamba, vita ni kukanusha
usawa. "Vita ni kunyimwa haki zote na uchokozi makubwa kwa ubinadamu na mazingira
Hivyo, kuna haja kwa dhamira hii, kuepuka vita kwa njia ya mazungumzo kama njia Mkataba
wa Umoja wa Mataifa, katika uwazi na ukweli kwa ajili ya amani na si kwa nia chinichini
zilizoficha nia tata. Aidha Papa alikemea kuenea kwa silaha akisema , "hapana kwa
silaha, hasa zile zenye kuleta maangamizi kwa wengi. Mwandamizi wa Petro alieleza
na kuonyesha kuridhishwa na moja kwa makubaliano ya hivi karibuni juu ya suala la
nyuklia ya Iran , na tena kile alichokiita kuwa matokeo mabaya ya uratibu wa hatua
za kisiasa na kijeshi, kati ya wanachama wa jumuiya ya kimataifa.
Papa aliigeukia migogoro dunia ya dunia kwa wakati huu, akisema "hawezi kuacha kutoa ombi lake kwa mara nyingine, kwa ajili ya hali za uchungu katika Mashariki ya Kati, Afrika Kaskazini na nchi nyingine za Afrika". Na alizungumzia jinsi chuki na "wazimu" unavyo sukuma mtu kuua, kuteka wengine, kuharibu sehemu za ibada na urithi wa utamaduni. Papa aliomba jumuiya ya kimataifa kufanywa uchunguzi wa ufahamu wa watu hao wanaoendesha vita na uharibifu. Papa Francisco aliitaja waziwazi migogoro inayoendelea Ukraine, Syria, Iraq, Libya, Sudan Kusini na katika Maziwa Makuu.Na aòlikumbusha kwamba, katika vita na migogoro ya kisiasa watu wanaoteseka zaidi ni ndugu zetu wanaume na wanawake, vijana na wazee, wavulana na wasichana, wasioweza kujitetea, ambao wanaugulia kilio cha mateso na kifo. Papa alieleza na kuomba Jumuiya ya Kimataifa itende wa ushupavu zaidi katika kuwalinda watu wasio na hatia. Na katika kukabiliana na majanga mengine kama janga la madawa ya kulevya, biashara haramu na unyonyaji wa watu", "rushwa" ambayo inajenga miundo yenye kutishia uaminifu wa taasisi.
Papa Francisko aliendelea kwa kufanya nukuu, katika hotuba iliyotolewa na Paulo
VI kwa Umoja wa Mataifa, ambamo alisema, hatari za maisha hutoka kwa watu wenyewe.
Papa Francisco, aliendelea kuzungumzia manufaa ya wote, haja ya kujenga udugu mzima
na kuheshimu utakatifu wa kila maisha ya binadamu. Familia ya kawaida pia lazima
kujengwa juu ya uelewa wa utakatifu wa asili uumbaji .Uelewa huu na heshima hii
zinahitaji kiwango cha juu cha hekima.
Papa ameitazama dunia ya kisasa iliyoungana kama kijiji, na inayo endelea kupanuka
kitandawazi lakini wakati huohuo pengo la migawanyiko na utengano vikizidi kukua katika
jamii. Papa aliusisitiza umoja wa Mataifa kwamba, hauwezi kujiweka mbali na baadhi
ajenda zinazotazama mustakabali wa dunia kwa siku zijazo. Hivyo kwa mara nyingine
, alirudia kutoa ombi lake la kuzitaka idara na itikadi zinazohusika , kuhudumia
kwa manufaa ya wote.
All the contents on this site are copyrighted ©. |