2015-09-25 10:31:00

Papa katika ibada ya Masifu ; awashukuru watawa wa Marekani


Baba mtakatifu Francisco Alhamisi akiongoza Ibada ya masifu ya Jioni katika Kanisa Kuu la kale la Mtakatifu Patrick, la Mjini New York, alionyesha kutambua kwamba, kanisa hilo ni matunda ya kazi ngumu ya watu wengi  wake kwa waume, waliyoyatolea maisha yao mhanga bila kujibakiza katika utumishi wa kanisa.  Na hivyo ameitaja kuwa ni  ishara nzuri ya kazi ya wahenga,  makuhani , watawa na walei aminifu wa Marekani,  waliosaidia kujenga Kanisa nchini Marekani.

Papa alitazama kwa kina, jukumu lao la msingi katika ujenzi wa jamii ya Marekani, na hivyo akatoa shukurani zake nyingi kwa  makuhani na watawa  ambao  hasa wamejikitika katika mipango ya  elimu na lishe katika taifa la Marekani. Alieleza na kutoa mfano wa mwanzilishi wa kwanza wa Shule Katoliki huru ya wasichana nchini Marekani, Mtakatifu  Elizabeth Ann Seton na Mtakatifu  John Neumann, mwanzilishi wa kwanza wa mfumo wa elimu Katoliki Marekani , akisema kwamba watu wengi kulipwa gharama za kafara ya ajabu na alifanya hivyo kwa kishujaa upendo.

Lakini pia hakuogopa kutaja moja kwa moja kasoro zilizo chafua sura nzuri ya Kanisa nchini Marekani,  kashfa  ya ngono kwa watoto, aibu iliyoletwa na watumishi wabovu wa Kanisa . Papa Francisko,  alikubali mateso ya wake kwa waume, na wale waliokubali kuibeba aibu ya unyama huu uliodhalilisha  ndugu hawa wanyonge  katika  Kanisa na kuwaweka katika mazingira magumu zaidi ... Papa amesema anatolea sala na faraja zake katika kwa wakati huu wa maumivu na uchungu wa moyo.

Na aliwarejea tena  Mapadre na watawa wa Marekani , akiwahimiza n akuwataka wawe watumishi wema, watumikie kwa uaminifu, furaha na kuridhika katika wito wao. Wafanya kazi kwa bidii na kuyaishi maisha ya kujinyima  na uaminifu kwa mujibu wa karama za waanzilishi wa jumuiya na mashirika yao kama  njia ya upendeleo katika kutoa jibu kwa Upendo wake Mkuu Yeye aliyewaita  katika kulitumikia Kanisa.

Kwa namna ya pekee, Papa aliendelea kutambua na kuonyesha heshima yake na shukrani kwa watawa wa kike nchini Marekani akihoji, bila wao utendaji wa Kanisa ungekuwaje hasa nchini Marekani. Alisifu kwamba, Wanawake wana nguvu, na kwa ujasiri huo, huwaweka mstari wa mbele katika kuitangaza Injili .

Alimalizia na shukurani kwa Watawa, masista na wanawake wote walioyatolea maisha yao katika kuifikisha habari njema katika kila kona ya taifa la Marekani na kwingineko duniani.  "Asante Sana ", na “ninawapenda wote”. 








All the contents on this site are copyrighted ©.