2015-09-21 10:37:00

Papa awaambia Mapadre na Watawa:Msiogope umasikini na ukarimu .


Jumapili akiwa ziarani  Cuba, Baba Mtakatifu Francisco baada  kutembelea jengo la Ikulu ya  Cuba, kwa muda mfupi alisimama katika Kanisa la Moyo Mtakatifu wa Yesu , lililodhaminishwa kwa Wajesuit. Na mara alikwenda katika Kanisa Kuu la Mjini Havana, la Mtakatifu Maria Asiyekuwa na doa,  kwa ajili ya  Ibada ya masifu ya jioni, ambako alisali sala hiyo akiwa pamoja na Maaskofu, Mapadre, Watawa na Waseminaristi. 

Baba Mtakatifu katika homilia yake alionyesha kuguswa na hotuba ya kumpokea katika Kanisa hilo , iliyotolewa na Kardinali Ortega , ambaye alizungumzia juu ya umaskini wa Kanisa la Cuba na pia Papa alisikiliza ushuhuda wa mtawa mmoja, juu ya kuishi na wagonjwa wasiojiweza na wagonjwa wa akili.

Mahali hapo Papa alishukuru,  si tu  kudra na huruma ya Mungu lakini pia alikumbuka  maisha ya baadhi ya wazee miongoni mwao, wenye kujua yote katika uzoefu wao wa maisha kwamba "huruma zake Mungu  ni za milele, na uaminifu wake ni wa karne zote". Papa alieleza na kutoa mwaliko kwa wote kumshukuru Mungu kwa ajili ya hilo.

Aidha Papa kwa namna ya kipekee alitoa shukurani kwa ajili uwepo wa Roho katika utajiri wa karama mbalimbali tofauti za wamisionari , waliofika katika nchi hiyo, watu waliozamia na kubobea na kuwa wananchi Wacuba miongoni mwa Wacuba, ishara inayoonyesha kwamba huruma ya Mungu ni ya milele.

Papa alieleza na kuendelea kutoa tafakari kwa somo la Injili akisema Injili ilikuwa inamwonyesha Yesu akiwa katika  mazungumzo na Baba yake . Na hivyo linaashirika muumini  kuzamisha kina cha moyo wa urafiki katika  sala, kama  mazungumzo ya baba na mwana.

Papa alikumbusha wote jinsi saa ya Yesu ilipofika,  aliomba kwa ajili ya wanafunzi wake , wali waliokuwa naye na wale wanaokuwa bado kufika , kama ilivyoandikwa katika Injili ya Yoh.17:20. Na kwamba katika wakati huo muhimu, Yesu aliunda mfumo wa maisha ya wanafunzi wake wote, kuwa ni mfumo wa sala na maombi kwa Mungu juu mbinguni .  Yesu aliifahamu vyema mioyo ya wanafunzi wake , na alimwomba baba yake awadumishe katika umoja naye..

Na hivyoYesu  aliomba kwa Baba  yake , awaokoe wafuasi wake dhidi ya  roho ya kutengana, roho ya kupapalika wakati wanapokabiliwa  matatizo na mashaka, moyo wa kutafuta faraja  katika mambo ya mpito na yaliyo tofauti na maadili na wengine na yenye kujenga moyo wa kujitenga.  Papa alieleza na kukemea moyo wa namna hiyo ndani ya kanisa akisema, moyo kama huo ndani , huweka  makunyazi katika  uso mzuri wa Kanisa. Hali hizo huongoza katika mfumo wa kujitenga , na uchovu, kwa huzuni polepole, hupandikiza  chuki, na malalamiko ya mara kwa mara, yenye kuleta uchovu . Hayo siyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yetu, wala si maisha yanayoongozwa na Roho Mtakatifu (Evangelii Gaudium, 2), kwa wale walioalikwa naye, alisisitiza.

Ndiyo maana Yesu anasali ili kwamba , maisha ya huzuni  na kujitenga yasijengeke  katika mioyo ya wafuasi wake.  Yesu anaomba na anatualika tena kuomba, kwa sababu anajua kuwa  baadhi ya mambo yanaweza tu kuwa uzoefu wa maisha kama zawadi.

Papa aliendelea kuzungumzia juu ya umoja  akisema ni neema iliyo  juu yetu yenye kufanikishwa na Roho Mtakatifu. Hivyo sisi tunapaswa kuiomba neema hii kwa ajili ya mabadiliko chanya katika maisha, mabadiliko yanayofanikishwa na Roho Mtakatifu kama  zawadi  kwetu.

Papa alifafanua na kuweka bayana kwamba, umoja, mara nyingi  huchanganywa na kufanana  au kua sare katika utendaji,  hisia na maneno. Lakini umoja haina maana ya kuwa sare katika kila jambo, bali ina maana ya kuwa na upendo mmoja kwa mwingine bila kujali tofauti zilizopo katika hisia na itikadi za mwingine. Na umoja mara nyingi huwekwa hatarini pale sisi tunapojaribu kuwaona watu wengine kuwa tofauti na sisi na hivyo kuwatenga au kuwabagua. Kumbe umoja ni zawadi, na si  jambo la kulazimisha kwa nguvu au kwa amri, lakini hujengwa na upendo wa kukaribiana na kukutana kama binadamu.  Papa alieleza na kutoa  mwaliko kwao wote , kumwomba Mungu hamu zaidi ya kukaribiana, mmoja kwa mingine. Kuwa majirani  daima, licha ya kutofautiana katika baadhi ya mambo, hiyo ni sehemu ya maisha.

Na aliwalenga moja kwa moja Maaskofu, Mapadre na wahudumu wa Kanisa akiwataka wawe  karibu na waamini. Wawe viongozi walio wazi na wenye kujali hoja na matatizo ya wengine.  Papa ameitaja migogoro na kutoelewana katika Kanisa, wakati   mwingine huhitajika kwa ajili  ya kuonyesha uhai wa kanisa na uwepo wa  Roho Mtakatifu kwamba yu hai na anafanya kazi zake . Papa alieleza na kukemea jamii ya  "ndiyo ndiyo " au ile daima  yenye kusema  "hapana kwa kila jambo"!.

Papa alikamilisha maelezo yake na ombi kwa Yesu, ambaye daima huruma yake  kamwe haifadhaishi, lakini daima huwa na  uwezo wa kurejesha furaha yetu. Na hili ni jambo  muhimu na la thamani kwa maisha ya watu wa Cuba. 








All the contents on this site are copyrighted ©.